Saturday, June 14, 2014
MADUDU KWENYE BAJETI 2014/2015
Do you like this story?
Serikali
imeendeleza usiri kuhusu gharama halisi za uendeshaji wa Bunge Maalumu la Katiba,
kutokana na gharama hizo kutowekwa wazi katika vitabu vyote vya makadirio ya
matumizi kwa mwaka wa fedha 2014/15.
Bunge
Maalumu la Katiba linatarajiwa kukutana kwa mara ya pili kuanzia Agosti, baada
ya kuahirishwa Aprili ili kupisha vikao vya Bunge la Bajeti ambavyo
vinaendelea mjini Dodoma hivi sasa.
Uchambuzi
uliofanywa katika vitabu vya bajeti unaonyesha kuwa fedha za kugharimia Bunge
la Katiba zimetengwa chini ya fungu namba 21 ambalo ni Hazina katika kipengele
ambacho kinajumuisha utekelezaji wa masuala mengine kadhaa.
Kitabu
namba mbili ambacho kimechambua makadirio ya matumizi ya Serikali kinaonyesha
kuwa zaidi ya Sh227.725 bilioni, zimetengwa chini ya kifungu namba 290700
kinachoitwa Contingency Non-Emergency (mambo yanayoweza kutokea ambayo siyo
dharura), huku ufafanuzi kwenye randama za Hazina zikionyesha Bunge la Katiba
ni moja ya mambo hayo.
“Matumizi
katika eneo hili yanajumuisha gharama za upigaji kura za maoni ili kupitisha
Katiba Mpya, kuboresha Daftari la Wapigakura kwa ajili ya uchaguzi ujao, kulipa
madeni ya makandarasi na watumishi na gharama za kuendesha Bunge la Katiba,”
inasomeka sehemu ya randama ambayo iliwasilishwa bungeni ikifafanua matumizi ya
fedha zilizoombwa na kuendelea:
“Makubaliano
mapya ya PAYE kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, nyongeza ya gharama za
shule, mitihani, bweni na ukaguzi wa shule za msingi na sekondari,
mchango wa Serikali kwenye capitation: gharama za ujenzi katika maeneo mapya ya
utawala, stahili za waajiriwa wapya katika mamlaka za serikali za mitaa.”
Maeneo
mengine yanayotajwa katika randama hiyo ni deni la michango ya watumishi wa
PSPF, mfuko wa jimbo, michango katika taasisi na mashirika ya kimataifa, deni
la HESLB kwa mfuko wa PSPF, deni la Ukumbi wa Bunge kwenye Mfuko wa NSSF, on
call allowance (posho) kwa ajili ya hospitali za mikoa na wilaya, pamoja na
madeni ya mashirika.
Hata
hivyo wakati kukiwa na maelezo hayo, randama za makadirio ya matumizi ya Wizara
ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi zinaonyesha kuwa Idara ya Ukaguzi wa Shule ambayo
inahusika na ukaguzi wa shule za msingi na sekondari imetengewa kiasi cha
Sh9,542,456,924 katika mwaka ujao wa fedha.
Kati
ya hizo Sh8,792,456,924 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na Sh750,000,000 ni
kwa ajili ya miradi ya maendeleo itakayojumisha ukaguzi wa shule na ukarabati
wa ofisi za ukaguzi wa shule katika Kanda za Ziwa na Nyanda za Juu Kusini na
Halmashauri za Wilaya za Bagamoyo, Sumbawanga, Hai, Urambo na Chunya.
Via<Mwananchi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “MADUDU KWENYE BAJETI 2014/2015”
Post a Comment