Thursday, June 5, 2014
MISS MBEYA 2014 KUPATIKANA KESHO.
Do you like this story?
![]() |
|
Mratibu wa Miss Mbeya Bi, Amani Mbilo
|
![]() |
| Pichani ni warembo waliowahi kushiri shindano hilo picha na maktaba |
Maandalizi ya
shindano la kumtafuta Miss Mbeya kwa mwaka 2014 yamefikia katika hatua za
mwisho ambapo kesho June 6 mwaka huu mrembo huyo anatarajiwa
kupatikana katika viwanja City Pub, ambapo warembo 11 watachuana jukwaani
kuwania taji hilo.
Akizungumza na
waandishi wa habari Jijini Mbeya Mratibu wa shindano hilo lililoandaliwa
na kampuni ya Bomba Fm Radio, Amani Mbilo, alisema mshindi katika
kinyang’anyiro hicho atazawadiwa kiasi cha shilingi 500,000.
Amesema mshindi wa
pili atapata kiasi cha shilingi 300,000, mshindi wa pili 200,000, huku
washiriki wote waliobaki wataambulia kifuta jasho cha fedha kama gharama ya
usafiri wa kufika katika mashindano hayo.
“Washiriki hawa 11
ni kutoka katika wilaya mbili tu za Mbeya City Centre na Mbeya Vijijini
kutokana na wilaya nyingine kukosa hamasa ya kuendesha mashindano haya hali
iliyosababisha ushiriki uwe wa wilaya mbili tu” alisema Mbilo.
Mratibu huyo
aliwataja washiriki hao 11 kuwa ni Meryam Cephas, Juliana Gilbert, Joanitha
Tibenderana, Matilda Hillu, Joyce Lameck.
Aliwataja washiriki
wengine kuwa ni Pendo Nelson, Atukuzwe Fabian, Anitha Patrick, Rhoda
Joseph, Felister Godion na Emiliana Abdalah.
Wadhamini katika
shindano hilo ni Tbl kupitia kinywaji cha Reds, Access Computer, Mbeya Peak
Hotel, Kihumbe, Air Tanzania na Dorcus Saloon.
Aidha, Mbilo alisema
katika shindano hilo litasindikizwa na burudani ya bendi ya muziki wa dansi
nchini la Fm Academia kutoka Jijini Dar es salaa na mgeni rasmi ni Kamanda wa
Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


.gif)



0 Responses to “MISS MBEYA 2014 KUPATIKANA KESHO.”
Post a Comment