Thursday, June 5, 2014
MKATABA MNONO WA MILIONI 360 ZA BINSLUM KUINOGESHA MBEYA CITY.
Do you like this story?
![]() |
| Wakuu wa idara mbalimbali wa halimashauri ya jiji la Mbeya wakiwa wanashuhudia tukio zima la kuweka saini katika Mkataba |
![]() |
| Mkurugenzi wa kampuni ya Bin Slum Tyre Company Limited Bw Mohamed Ahmed Binslum akiweka saini Mkataba |
![]() |
| Mwanasheria wa jiji akiwa anaweka saini katika mkataba |
![]() |
| Waandishi wa Habari wakichukua tukio zima la kusaini Mkataba |
Hatimaye
Timu ya Mbeya City inayomilikiwa na Halmasahuri ya jiji la Mbeya
ambayo inashiriki ligi Tanzania bara leo imewka saini katika mkataba mnono kwa
ajili ya kudhamni Clabu hiyo wa sh.milioni 360 kwa miaka miwili kutoka
kampuni ya Binslum ya Jijini Dar es salaam.
Mbeya City
iliyojizolea sifa lukuki kwa mtindo wake wa kuzizidi timu zote zilizocheza ligi
Kuu msimu uliopita imewashawishi wadhamini hao kuwekeza kwa timu hiyo kwa nia
ya kuongeza chachu kwa timu za mikoani zinazocheza Ligi Kuu.
Akizungumza
wakati wa kuweka saini mkataba huo katika ukumbi wa Halmashauri ya Jiji leo
asubuhi, Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Mohamed Binslum amesema udhamini wao
umelenga kuleta changamoto na hamasa kwa timu za mikoani.
Binslum
amesema kuwa wameamua kuwekeza kwa Timu ya Mbeya City kutokana na namna ambavyo
timu hiyo imeonesha mtindo wa kipekee wa ushawishi kwa soka hapa nchini kinyume
na ilivyozoeleka kwa timu kubwa za Yanga na Simba.
Alisema
kuwa kampuni ya Binslum inaamini itanufaika kwa kutangaza bidhaa zake kupitia
jezi za timu hiyo katika michezo yake kwa msimu wa mwaka 2015-16 na kuwa
wamefikia makubaliano hayo na uongozi wa Mbeya City kutokana na mwitikio mkubwa
wa wapenzi wa soka katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini.
Awali
akizungumza katika hafla hiyo fupi ya utiaji saini mkataba na kampuni hiyo
Meneja Mbeya City Emmanuel Kimbe amesema kuwa anaamini ufadhili huo utachangia
kuiongezea uwezo timu hiyo katika ligi Kuu msimu ujao wa 2015 na 2016.
Amesema
kuwa mkataba huo utachangia kuongeza kipato cha timu hiyo na kuiwezesha
kujikimu kwa matatizo madogo madogo ambayo anaamini yatatatuliwa kwa ufadhili
huo wa miaka miwili.
Naye Kaimu
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya ambaye ndiye mmiliki wa timu hiyo
Dkt. Samwel Lazaro amesema kuwa ufadhili kwa timu za mikoani utachangia klabu
nyingi zisizo na uwezo wa kifedha kushiriki ligi kwa ushindani katika ligi na
kukua kwa soka la Tanzania.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


.gif)











0 Responses to “MKATABA MNONO WA MILIONI 360 ZA BINSLUM KUINOGESHA MBEYA CITY.”
Post a Comment