Friday, June 13, 2014
UJUMBE HUU ALIOUTOA MONALISA KWA WALE WANAODAI HASTAHILI KUPOKEA POLE ZA GEORGE TYSON UNAUMIZA KWA KWELI
Do you like this story?
Muigizaji wa filamu nchini Yvonne
Cherry maarufu kama Monalisa ambaye pia aliwahi kuwa mke wa marehemu George
Tyson aliyefariki dunia kwa ajali ya gari wiki kadhaa zilizopita, amefunguka
kupitia Instagram kuelezea kusikitishwa kwake na majungu ya watu kuwa
hakustahili kupewa pole kufuatia msiba huo.
Monalisa ameandika: /Let me clear the
air.ni hivi,pamoja na ujinga tulioufanya mimi na George ktk maisha yetu,kwa
macho ya kibinadamu utasema alikuwa na mke mwengine..bt kwa macho ya kiMungu
mimi ni mke halali wa George Otieno Okumu aliyelala.anayesema mke wa tyson
alijifungia ndani mm nikawa nachukua pole zisizo zangu,dah!kwanza wanawake
walikuwa wawili ndani sio mmoja.na wote walijifungia ndani,kwanini?ni wakristo
na wanaijua dini.waombolezaji waliokuwa wakinipa pole mimi,ni kwann?jiulize
kabla ya kuropoka halafu ww ni mwanamke kuna siku yatakukuta.nilienda kutimiza
wajibu wangu kama mke,ningelia peke yangu kwetu mngenisema sana,nimekaa msibani
naambiwa nachukuwa pole za bure.wacha nikukumbushe maandiko 'Alichokiunganisha
Mungu?.;kilichofungwa duniani?"¦..;nikupende,nikutunze hadi kifo?¦.. sasa
kifo kimetutenganisha.siku ya mwisho unadhani George ataitwa na nani?pamoja na
mambo yake yote wacheni nimlilie he was a good father kwa Sonia wangu esp.miaka
5 ya mwisho wa uhai wake.acheni nimlilie he was my best friend
1998-2014.nimeshare nae kitanda 2000-2006.nitakuwa mtu wa aina gani nisiwe na
uchungu?ukiona mwanamke mwenzio kaishindwa ndoa usimcheke jua kuna sababu..na
ni fundisho kwa wachukua waume za watu wote mjini,mume akiumwa huwa anarudi kwa
mkewe,na akifa?and for ur info..msianze anajifanya mke ss hv ili apewe
mali..Sonia ni mali kubwa sana alioniachia am so happy.waaache wao wanaolilia
kupewa pole wapiganie.mwenyewe aliyetafuta kafa kaziacha sembuse
tuliobaki?niacheni nimlilie,waacheni fans wangu walie na mm.
George Tyson anatarajiwa kuzikwa
Jumamosi ya June 15 kwao Kisumu Kenya.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ UJUMBE HUU ALIOUTOA MONALISA KWA WALE WANAODAI HASTAHILI KUPOKEA POLE ZA GEORGE TYSON UNAUMIZA KWA KWELI ”
Post a Comment