Wednesday, November 12, 2014
BASI LAPINDUKA, LAUA NA KUJERUHI ASUBUHI HII.
Do you like this story?
Watu kadhaa wamepoteza maisha huku wengine
wakijeruhiwa asubuhi hii kwenye ajali ya basi la Wibonela lililokuwa likitoka
Kahama kwenda Dar lililopinduka eneo la kona ya Phantom, Kahama.
Chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi uliopelekea dereva wa basi kushindwa kulimudu lilipofika kwenye kona ya Phantom na kupelekea kuingia mtaroni na kupinduka.
Idadi kamili ya waliopoteza maisha na majeruhi kwenye ajali hiyo bado
haijafahamika.
Baadhi ya miili tayari imetolewa katika eneo la ajali huku majeruhi nao
wakikimbizwa kwenye Hospitali ya Wilaya Kahama kwa matibabu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ BASI LAPINDUKA, LAUA NA KUJERUHI ASUBUHI HII.”
Post a Comment