Friday, November 14, 2014
HATURUHUSU WAFUNGWA KUFANYA TENDO LA NDOA GEREZANI,WIZARA YA MABO YA NDANI.
Do you like this story?
SERIKALI imesema Tanzania haina sheria ya kuwaruhusu wafungwa kukutana faragha na wenzao wao.
Hii ni mara ya tatu
kwa serikali kutoa majibu hayo, kutokana na maswali ya wabunge ambapo mara
kadhaa swali hilo limekuwa likiulizwa na Mbunge wa Viti Maalumu, Maryam Salum
Msabaha (Chadema).
Hata hivyo, jana
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima alikiri kwa Tanzania
kutokuwa na sheria hiyo na akajibu kuwa ujauzito ambao huwapata wafungwa
wanawake, unatokana na wafungwa hao kuupata nje ya Magereza.
Kauli hiyo aliitoa jana
bungeni alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Maalumu, Rukia Kassim Ahmed (CUF)
ambaye alitaka kujua ni kwa namna gani wafungwa wanawake wanapata ujauzito
wanapokuwa ndani ya magereza yao.
Pia, alihoji kama
magerezani kuna usiri, ni kwa namna gani mahabusi ambao ni mashekhe kutoka
Zanzibar wanafanyiwa vitendo vya ulawiti gerezani.
Akijibu swali hilo,
Naibu Waziri huyo alisema jeshi la Magereza lina utaratibu wa kutenganisha
wafungwa wa kiume na wa kike kwani kila watu hutunzwa kwa sehemu zao na hulindwa
na watu wa jinsia zao.
Kuhusu tuhuma za
kulawitiwa kwa mashekhe wa Zanzibar, Waziri wa Mambo ya Ndani Mathias Chikawe,
alisema sakata la Shekhe Salum Ali Salum linafanyiwa kazi na kwamba kiongozi
huyo ameshafanyiwa uchunguzi wa awali katika Hospitali ya Amana.
“Jambo hilo lipo mikononi mwetu,
tumempeleka Hospitali ya Amana na kesho (leo) tutampeleka Hospitali ya
Muhimbili kwa uchunguzi zaidi, lakini tunachunguza pia tabia ya kiongozi huyo
na mwenendo wake kabla ya kuingia gerezani,”
alisema Chikawe.
Hata hivyo, Chikawe
alisema kumekuwa na mkanganyiko mkubwa kwa watuhumiwa hao, kwani tangu mwanzo
hakuwa ameripoti vitendo hivyo, lakini alipofika mara ya nne gerezani ndipo
akaripoti kufanyiwa vitendo hivyo na mmoja wa polisi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “HATURUHUSU WAFUNGWA KUFANYA TENDO LA NDOA GEREZANI,WIZARA YA MABO YA NDANI.”
Post a Comment