Friday, November 14, 2014
SERIKALI IMETOA KAULI KUHUSU VOCHA KUISHA HARAKA KWENYE SIMU.
Do you like this story?
Watumiaji wengi wa
huduma ya simu za mkononi wamekuwa wakilalamikia wizi wa pesa unaofanywa na
baadhi ya makampuni hayo, leo katika kikao cha Bunge Dodoma Serikali
imesema inatambua kuhusu wizi unaofanywa na baadhi ya makampuni ya simu
za mkononi na kutoa tamko namna ambavyo imejipanga kukabiliana na wizi wa aina
hiyo.
Akitoa tamko hilo
Naibu Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Teknolojia January Makamba amesema
Serikali itaanzisha kituo maalum cha kushughulikia malalamiko hayo CCC,
kitakachokuwa kinasimamiwa na TCRA.
Akiuliza swali
kuhusiana na jinsi Serikali ilivyojipanga kukabiliana na wizi huo Mbunge
wa Konde Khatib Said Haji amesema; “… Wizi huu unaofanywa na makampuni ya simu
si wizi mkubwa kama ule wa ESCROW.. ni wizi mdogo mdogo unaowaibia
Watanzania elfu tano elfu tatu lakini kwa ujumla wake, Mpemba aliyeko Konde
akiibiwa elfu tatu, Mnyamwezi wa Tabora elfu mbili, Ukizijumlisha ni mamilioni
ya shilingi wanaibiwa Watanzania… Leo watu hao elfu tatu elfu mbili unawaambia
wapeleke malalamiko yao, gharama hiyo umeikadiriaje hata mtu huyo akadai
malalamiko ya elfu tatu..”
“.. Hivi serikali
yenu makini imekuwa wapi muda wote mpaka kukiri kama Watanzania wamekuwa
wakiibiwa na bila wenyewe kujijua?, na bado hamna hatua mlizozichukua, ni nani
aliyeko nyuma ya pazia hili la kuibia Watanzania na ninyi mkaridhia ama ni yale
yaliyosemwa kama CCM ina fund katika wizi huu..?”- Khatib Said Haji.
Akijibu swali hilo
Naibu Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Teknolojia January Makamba amesema; “…Napenda
nikiri tatizo la wizi au dhuluma kwa wateja lipo na ndio lililopelekea tukaweka
hizi kanuni ambazo zinaweka adhabu na hatua za kuchukua katika kuchukua katika
kudhibiti wizi huo.. Licha ya utaratibu wa kawaida wa kulalamika katika
makampuni ya simu, kwa sababu moja ya matakwa ya sheria ni kwamba kampuni
za simu zinapaswa kuweka utaratibu wa kuhudumia watekja wake, lakini tumebaini
kwamba utaratibu huo una matatizo, unaweza ukapiga simu muda mrefu
isipokelewe, unaweza kuambiwa usubiri na wakati unasubiri kulalamika pia
unakatwa..
Kwa hiyo Serikali
inafahamu hilo, pamoja na hatua tulizozichukua ni kuweka ule mtambo wa
kufuatilia mawasiliano ambao moja ya kazi yake sio kufuatilia tu mapato lakini
ubora wa mawasiliano.. Kwa kutambua kuwa makampuni ya simu haya wakati mwingine
yanachelewa wakati mwigine yanapuuza wateja, kituo hiki ambacho tunakianzisha
namba zake zitasambazwa kila mtu atakuwa nayo, kwa hiyo huna haja kusafiri
kufuatilia shilingi elfu mbili elfu tatu elfu tano. Kutakuwa na namba ambayo ni
bure kupiga..”- January Makamba.
“ Kila utakapopiga
kulalamika utapewa namba maalum ya lalamiko lako, na lisiposhughulikiwa hata
kitengo cha kampuni ya simu kutoshughulikia lalamiko lako na yenyewe itakuwa
sababu ya makampuni hayo kuadhibiwa..”- January Makamba.
Unaweza kusikiliza
majadiliano juu ya suala hilo hapa kama ilivyokuwa katika kikao cha bunge leo
Dodoma.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “SERIKALI IMETOA KAULI KUHUSU VOCHA KUISHA HARAKA KWENYE SIMU.”
Post a Comment