Friday, November 14, 2014
CHEZEA MUSSA AZZAN ZUNGU WEWE...ANGALIA ALICHOKIAMUA BUNGENI HUKO DODOMA
Do you like this story?
Kama hukupata nafasi
ya kufuatilia kilichokuwa kinaendelea Bungeni Dodoma jana, mambo makubwa matatu
ambayo Wabunge walihoji ni haya; kwanza kuhusu IPTL na akaunti ya ESCROW, pili
kuhusu mapigano ya wakulima na wafugaji Kiteto na tatu ni suala la mwenendo wa
Serikali kusuasua.
Mwenyekiti wa Bunge
hilo Mussa Azzan Zungu ametoa majibu haya;- “… Kamati ya uongozi wa Bunge
ilikuwa na kikao leo alhamisi tarehe 13 Novemba mwaka 2014, kuanzia saa 7
mchana na kufanya maamuzi muhimu kuhusiana na miongozo iliyoombwa bungeni leo
asubuhi kama ifuatavyo. Kuunda kamati teule ya Bunge kushughulikia suala la
IPTL na akaunti ya ESCROW.
Katika kujadili
mwongozo huu ambao uliombwa na Mheshimiwa Peter Serukamba, kamati ya uongozi
imekubaliana na taarifa ilitolewa na serikali kuwa mheshimiwa Waziri Mkuu
kesho atakabidhi kwa Spika ripoti ya CAG kuhusu suala hilo, baada ya
kupokelewa, utaratibu wa kawaida wa kibunge utafuata kuipatia kamati ya hesabu
za Serikali, PAC…”
Kuhusiana na mauaji
yaliyotokana na mapigano ya jamii za wakulima na wafugaji Kiteto,
mwenyekiti huyo amesema; “…. Katika kujadili suala hili ambalo mwongozo wake
uliombwa na David Silinde kamati imeazimia kwamba Serikali kupitia Waziri Mkuu
itoe maelezo kwa kamati ya uongozi kesho jioni juu ya jambo hili na namna
lilivyoshughulikiwa kuanzia kipindi cha nyuma hadi sasa. Na kisha taarifa
kamili kuhusu suala hilo itatolewa Bungeni….”
Suala la tatu ni
kuhusu mwenendo wa Serikali kusuasua, Mwenyekiti Zungu amesema; “…. Katika
kujadili mwongozo huu ambao ulitolewa Bungeni na Mheshimiwa Rajabu Mbarouk
Mohammed, kamati ya uongozi iliazimia kwamba suala hili lijadiliwe katika kikao
cha kamati ya uongozi pamoja na Waziri Mkuu kitakachofanyika kesho jioni….”
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ CHEZEA MUSSA AZZAN ZUNGU WEWE...ANGALIA ALICHOKIAMUA BUNGENI HUKO DODOMA ”
Post a Comment