Wednesday, December 17, 2014

AKAMATWA KWA KUGHUSHI BIMA YA AFYA




Mtu mmoja aliyejifanya kuwa ni mfanyakazi wa Taasisi ya IMTU, Bakari Ramadhani amekamatwa na maofisa wa Shirika la Taifa la Bima ya Afya (NHIF), akiwa na fomu zao za kughushi za kuchukulia dawa zikiwa zimegongwa mihuri inayoonyesha ni ya Hospitali ya Rufaa ya Temeke.


Ramadhani ambaye ni mkazi wa Kinondoni Mosco, alikamatwa jana ndani ya duka la J.D anakodaiwa kwenda mara kwa mara kuchukua dawa. Inadaiwa mtu huyo pia ameshafanya hivyo mara kadhaa mpaka kwenye matawi ya duka hilo. Aliwekewa mtego na maofisa wa NHIF kwa kushirikiana na wafanyakazi wa duka hilo na wakafanikiwa kumkamata.

Ramadhani ameiambia Fahari News kuwa anachukua dawa hizo kwa ajili ya kuwasaidia ndugu zake 15 ambao ni wagonjwa.

Alisema amekwisha chukua dawa kwa mtindo huo katika matawi ya duka la J.D ya Mlimani City, Kariakoo na Posta. Aliyataja maduka mengine kuwa ni Nakiete Mwenge na Okinawa lililoko Temeke.

0 Responses to “ AKAMATWA KWA KUGHUSHI BIMA YA AFYA ”

Post a Comment

More to Read