Thursday, December 18, 2014
MSWAADA TATA WAZUA VURUGU BUNGENI KENYA
Do you like this story?
Wabunge wa
Kenya wametofautiana pakubwa bungeni kufuatia mjadala kuhusu mswaada tatanishi
wa usalama ambao wabnunge w aupinzani wanasema unakiuka uhuru wa wakenya.
Bunge lililazimika kuahirisha vikao vyake kwa dakika
30 badala ya kujadili mswada tatanishi kuhusu usalama wa nchi. Kikao cha leo
kilikuwa kikao maalum ambacho kilipaswa kupitisha mswada huo ambao baadaye
utaidhinishwa na Rais kuwa sheria.
Wabunge wa upinzani wlaipinga mswada huo na kuanza
kurusha karatasi sakafuni huku wakitatiza shughuli bungeni humo.
Mwenyekiti wa kamati ya usalama wa bunge, Bwana Asman Kamama,
alijaribu kuyaja mabadiliko yaliyopendekezwa kufanyiwa mswada huo lakini
wabunge walianza kuimba na kumzomea spika wa bunge wakiukataa mswada huo
wakisema 'bado mapambano.'
Spika wa bunge Justin Muturi wakati mmoja alimuru
walinzi wa bunge kuwaondoa baadhi ya viongozi waliofika bungeni humo kwa
mjhadala ambao ulitarajiwa kuwa kaa moto, hasa kw aupande wa upinzani.
Mswada huo ambao umewasilishwa bunge kufuatia matukio
ya utovu wa usalama na mashambulizi nchini Kenya, unapendekeza kuwa washukiwaw
augaidi wanaweza kuzuiliwa kwa mwaka mmoja huku polisi wakifanya uchunguzi.
Via>BBC
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “MSWAADA TATA WAZUA VURUGU BUNGENI KENYA”
Post a Comment