Thursday, December 17, 2015
MADIWANI WATAKIWA KUBUNI NJIA ZA KUJIINGIZIA MAPATO,ABBAS KANDORO
Do you like this story?
| Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro |
NA
SAMWEL NDONI, ILEJE
MKUU
wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro amewashauri madiwani wanaounda Baraza la
Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Ileje kubuni miradi mbalimbali ya
kuliingizia kipato ili waweze kuwa na bajeti isiyotegemea msaada kutoka
Serikali kuu.
Kandoro
alitoa ushauri huo katika mkutano wa kwanza wa baraza la madiwani hao, ambapo
alisema kuwa endapo madiwani hao watakuwa na vyanzo vingi vya mapato wataweza
kuharakisha shughuli za maendeleo ya wilaya hiyo.
Alisema
kuwa mpaka sasa Bajeti ya Halmashauri ya Wilaya ya Ileje, ni kwakiasi kikubwa
huku akidai kuwa asilimia 92 ya bajeti hiyo inategemea fedha kutoka katika tegemezi
serikali kuu, hali ambayo alidai inafanya wilaya hiyo isipate maendeleo haraka
kama ilivyo kwa wilaya zingine za mkoa wa Mbeya.
Aidha
katika mkutano huo wa baraza la Madiwani hao ulifanyika uchaguzi wa Mwenekiti
na makamu mwenyekiti wa Halmashauri hiyo pamoja na uundwaji wa kamati mbalimbali za maendeleo.
Katika
uchaguzi huo Diwani wa Kata ya Bupigu kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM),
Ubatizo Songa, alichaguliwa kuwa mwenyekiti mpya wa Halmashauri hiyo kwa kupita
bila kupingwa, ambapo alipigiwa kura za ndio 24 zilizompa nafasi yakuweza kuiongoza
Halmashauri hiyo kama Mwenyekiti.
Katika
nafasi ya Makamu Mwenyekiti, diwani wa kata ya Isongole pia kupitia CCM,
Gwalusako Kapesa, alipita bila kupingwa kama ilivyokuwa kwa mwenyekiti na
kupigiwa kura za ndio 24.
Wagombea
wa CCM katika Halmashauri ya Wilaya ya Ileje walipita bila kupingwa kutokana na
vyama vya upinzani kuwa na Mgombea mmoja pekee kutoka Chadema, ambaye ni Diwani
wa kata ya Chitete.
Baada
ya kufanyika kwa Uchaguzi huo, Mkuu wa Wilaya ya Ileje, Rosemary Senyemule,
aliwataka madiwani hao kuwajibika ipasavyo ili kuendana na kasi ya Rais Dk.
John Magufuli ambaye katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25 alipata kura nyingi
katika Wilaya hiyo kuliko katika Wilaya nyingine zote za mkoa wa Mbeya.
Senyamule
alisema ili kudhihirisha kuwa kura ambazo wananchi wa Ileje walimpigia Dk.
Magufuli pamoja na madiwani hao zilikuwa ni za maendeleo ya wananchi wafanye
kazi kwa bidii ili wananchi wafurahie matunda ya kura zao.
Wilaya
ya Ileje ina jumla ya kata 18 ambapo katika Uchaguzi Mkuu wa Mwaka huu, Chama
cha Mapinduzi kilipata Jumla ya kata 17 huku Chama cha Demokrasia na Maendeleo
(Chadema) kikiambulia kata moja hali iliyokifanya CCM kuongoza Halmashauri hiyo
bila kupingwa.
Mwisho.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


.gif)

0 Responses to “MADIWANI WATAKIWA KUBUNI NJIA ZA KUJIINGIZIA MAPATO,ABBAS KANDORO”
Post a Comment