Thursday, December 18, 2014
TIBAIJUKA AGOMA KUJIUZULU
Do you like this story?
NA
CHALILA KIBUDA WA MICHUZI BLOG
WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Makazi,Profesa Anna Tibajuka
amesema kuwa hawezi kujiuzulu katika nafasi ya uwaziri kutokana fedha ya
Tegeta ESCROW.
Akizungumza
na Waandishi na Habari mapema leo jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa Hoteli
ya Hayyat Regency,Anna alisema kuwa udalali wake fedha hiyo ni kwa ajili ya
wanafunzi katika shule za Taasisi ya Johansson Girls
Education Trust.
Alisema fedha hiyo aliyoipata ni ni bil 1.66 ambazo zilitoka
katika kampuni ya James Rugemalira ni kwa ajili ya msaada wa shule za
Taasisi ya Johansson Girls Education Trust .
Alisema kuwa fedha hiyo kuingia katika akauti yake binafsi
ilitokana na masharti ya mtoa msaada ndugu James Rugemalira ambaye
alitaka fedha hiyo iingie katika akauti ya Benki ya Mkombozi. ‘’Nikijiuzulu
hata Rais Jakaya Kikwete atanishangaa kwani fedha nilizopata ni za shule na kwa
ajili kukomboa elimu nchini hasa kwa watoto wa kike kutokana na wazazi
wengi kutoweza kumudu gharama za shule’’alisema Anna.
Alisema kuwa udalali wake ni kutafuta fedha kwa ajili
ya elimu nchini ambapo, alidai hata Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP
,Reginard Mengi alitoa sh.milioni 248 kwa ajili ya msaada wa shule hiyo.
Anna alisema kuwa wananchi watambue kuwa yeye ni
mstaafu wa Umoja wa Mataifa hivyo hawezi kufanya hivyo na kama angetaka fedha
hiyo angeweza kufuata hata katika shule na kuchukua.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ TIBAIJUKA AGOMA KUJIUZULU ”
Post a Comment