Wednesday, January 7, 2015
AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MAISHA JELA KWA KOSA LA KUMLAWITI MTOTO WA MIAKA 5
Do you like this story?
Na Joachim Nyambo,Mbarali.
MAHAKAMA ya wilaya ya
Mbarali mkoani Mbeya imemhukumu kifungo cha maisha jela mkazi wa Madibira
wilayani hapa kwa kosa la kumlawiti mtoto mwenye umri wa miaka mitano.
Aliyehukumiwa kutumikia
kifungo hicho ni Samwel Mnyonge(30) ambapo hukumu hiyo imetolewa na hakimu
mfawidhi wa mahakama ya wilaya ya Mbarali Guwai Sumaye.
Awali ilidaiwa
mahakamani hapo na mwendesha mashitaka wa jeshi la polisi Mazoya Luchagula
mbele ya hakimu mfawidhi Sumaye kuwa mshitakiwa alitenda kosa hilo Februari
11,2014 kijijini Madibira wilayani hapa.
Mazoya alisema awali
mshitakiwa alimbeba mtoto huyo wa umri wa miaka mitano kwenye baiskeli akiwa
amempa msaada wa kumrejesha nyumbali alipokuwa akitokea shuleni lakini wakiwa
njiani,Mnyonge alimpeleka mtoto kwenye shamba la mahindi na kumlawiti.
Alisema kutokana na
majeraha makubwa aliyoyapa mtoto huyo,ilibidi ndugu na jamaa kumkimbiza katika
hospitali ya Mafinga wilayani Mufindi mkoani Iringa na baadaye mtoto huyo
kupelekwa hospitali ya Muhimbili jijini Dar es salaam alikokaa kwa muda wa
miezi nane kwaaajili ya matibabu.
Akitoa hukumu baada ya
kuridhishwa na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo,hakimu mfawidhi Guwai Sumaye
amesema anamhukumu Mnyonge kwenda jela kutumikia kifungo cha maisha ili iwe
fundisho kwa wengine wenye tabia hiyo.
Mwisho.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MAISHA JELA KWA KOSA LA KUMLAWITI MTOTO WA MIAKA 5”
Post a Comment