fahari News
Habari | Michezo | Bishara | Zabuni
Home
BIASHARA
KITAIFA
KIMATAIFA
USA
AFRIKA
AFRIKA MASHARIKI
MICHEZO
MUZIKI
SIASA
Recommended:
Perfect Social Media Marketing Stratergy For Your Business
Like
Saturday, January 3, 2015
PANYA ROAD WATIKISA JIJI LA DAR
Tweet
Share
Do you like this story?
KIKUNDI kinachodaiwa kuwa Panya Road kimetikisa maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam kwa kupora mali, kujeruhi watu na kuzua sintofahamu katika maeneo ya jiji hilo wakiwa na mapanga mikononi.
Maeneo yaliyokumbwa na dhooruba hiyo ni pamoja na Sinza, Tandale, Mwananyamala na maeneo mengineyo usiku wa kuamkia leo. Maduka na baa zilifungwa na kupelekea polisi kupiga risasi hewani kuwatawanya watu waliokuwa wamekaa kimakundimakundi.
Imeelezwa kuwa fujo zilianzia mchana jana baada ya kiongozi wa Panya Road aitwaye Diamond kuuawa maeneo ya mpakani mwa Tandale na Mwananyamala darajani usiku wa kuamkia mwaka mpya kwa kukatwakatwa na mapanga.
Baada ya kumzika mwenzao jana Mburahati Jijini Dar, vijana hao wakajipanga kwa ajili ya kufanya fujo.
Usiku ulipoingia wa jana wakaanza kazi na kusababisha taharuki kwa wakazi wa Jiji la Dar.
Baadhi ya mashuhuda walioshuhudia matukio hayo wanadai vijana hao walikuwa na silaha mbalimbali yakiwemo mapanga na walivamia maeneo kadhaa zikiwemo baa.
Wateja waliokuwa katika baa ya Calabash iliyopo maeneo ya Mpakani, Mwenge walilazimika kuacha vinywaji vyao na kukimbia hovyo huku wengine wakikanyagana na kukatwa na vipande vya chupa kwa kile kilichodaiwa kuwa vijana hao walikuwa wanakatiza maeneo hayo japo hawakuingia ndani.
Baada ya tukio hilo wateja wengi waliamua kurudi majumbani kutokana na baadhi yao kujeruhiwa na vipande vya chupa wakati wakikimbia.
0 Responses to “ PANYA ROAD WATIKISA JIJI LA DAR”
Post a Comment
Newer Post
Older Post
Home
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Tweets by @FahariNews
More to Read
Buzz
Twitter
Facebook
RSS
Email
Must Read
Popular Posts
MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI WA JESHI LA POLISI.
Jeshi la Polisi Tanzania linawaita kwenye usaili vijana waliomaliza kidato cha nne mwaka 2013 na kidato cha sita mwaka 2014 ambao w...
UBOVU WA BARABARA WAKATI WA MASIKA WAPELEKEA CHANJO KUCHELEWA KUFIKA KWA WAKATI KWENYE ZAHANATI WILAYANI MAKETE.
Katibu tawala wilaya ya Makete Joseph Chota ambaye alikuwa mgeni rasmi katika uzinduzi huo kwa niaba ya mkuu wa wilaya ya Makete, akito...
MECHI 6 AMBAZO HUTAKIWI KUZIKOSA MICHUANO YA CHAN 2016
Zimebaki saa chache kabla ya michuano ya CHAN 2016 kuanza kutimua vumbi inchini Rwanda. Nchi wenyeji watafungua michuano hiyo dhidi ...
PICHA : RAIS MAGUFULI AVAA SARE ZA JESHI AKIWA ARUSHA
Amiri Jeshi Mkuu, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na wananchi wa Arusha Mjini wakati akip...
TUNATAKA KAMPENI ZA AMANI NCHINI KOTE.
Tuanze makala haya kwa kumsifu Mungu, muumba wa vitu vyote vinavyoonekana na visivyoonekana katika dunia hii. Hakika tumhimidi daima...
0 Responses to “ PANYA ROAD WATIKISA JIJI LA DAR”
Post a Comment