Friday, February 6, 2015
WANAWAKE WAJANE WA KIMASAI WAANGUA VILIO HUKO MOROGORO
Do you like this story?
Wanawake wajane ambao
ni Wafugaji jamii ya Kimasai, wamejikuta wakiangua kilio katika kituo cha
Polisi Mvomero, mkoani Morogoro baada ya kukabidhiwa idadi pungufu ya ng’ombe
zilizokamatwa baada ya kuporwa na kundi la ulinzi wa jadi la wakulima.
Walinzi hao wa jadi
kutoka katika kijiji cha Dihombo, lilivamia
Kijiji cha Kambala ambacho wanaishi wafugaji hao na kupora ng’ombe 145 kwa
madai kuwa wafugaji wa kijiji hicho kuwapora wakulima wenzao pikipiki tatu na
kusababisha uhalibifu wa trekta wakati wakielekea shambani katika bonde la
Mgongola na pikipiki hizo kutelekezwa porini.
Mmoja wa wanawake
hao, Belitha William, alisema akiwa
kijijini Kambala akiendelea na shughuli za kuchunga mifugo yake, ghafla
alivamiwa na kundi la vijana wenye silaha za jadi maarufu kama muano na kupora
ng’ombe wake wapatao 145 pamoja na ndama na kuondoka nao.
Mfugaji huyo alisema
alipoifuatilia mifugo hiyo alielezwa inalindwa na kundi la walinzi wa jadi
mpaka pale wafugaji wa jamii hiyo ya kimasai watakaporudisha pikipiki
walizopora wafugaji wenzao.
Hata hivyo, alisema
baadaye mifugo hiyo ilipelekwa ofisi ya Tarafa ya Mvomero kwa ajili ya kupigwa
faini mifugo hiyo kuzurura katika mashamba huku mingine ikiwa haipo.
Kwa upande wao,
wakulima walioporwa pikipiki hizo, Fabian
Clement pamoja
naFrancis Boniface, wakielezea
tukio la kuporwa pikipiki hizo, walisema kwa nyakati tofauti kuwa wakati
wakielekea katika mashamba ya bonde la Mgongola kwajili ya kuwapelekea chakula
wenzao, waliona kundi kubwa la wafugaji jamii ya Wamasai wakiwa na silaha za
jadi pamoja na bunduki likiwafuata ndipo walipokimbilia porini.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “WANAWAKE WAJANE WA KIMASAI WAANGUA VILIO HUKO MOROGORO ”
Post a Comment