Tuesday, October 27, 2015
ALICHOKISEMA MCHEKESHAJI KINGWENDU BAADA YA KUSHINDWA UBUNGE KISARAWE.
Do you like this story?
Mwigizaji
Kingwendu ni miongoni mwa mastaa wa Tanzania ambao walichukua headlines
za kugombea ubunge kwenye uchaguzi mkuu 2015 ambapo wengine ni pamoja na Afande
Sele, Professor Jay na Mwigizaji Frank.
Mwigizaji/Mchekeshaji
Kingwendu hakufanikiwa kushinda kwenye kura za ubunge huku tiketi
yake kulitaka Bunge ikiwa inapitia CUF jimboni Kisarawe mkoa wa Pwani.
Baada
ya kushindwa, Kingwendu amesema ‘Kiukweli kabisa matokeo ya mwanzo kabisa
ilikua inaonyesha mimi naongoza lakini baada ya kumaliza kuhesabu kura
ikaonekana amenishinda yule bwana Suleiman Jafo wa CCM‘
‘Nimejaribu
na nimethubutu kwa mara ya kwanza kugombea nafasi kubwa ya Ubunge.. nimeenda
vizuri tu na sitachoka na wala sitaacha, najipanga tena kwa mara nyingine najua
nimekosea wapi na ntajipanga upya na ntaenda kusomea siasa zaidi‘–
Kingwendu
‘Mwaka
2020 huko nadhani nitakua niko sawa, nakwenda kusomea siasa zaidi ili niijue
siasa zaidi na nijue nitamkamata wapi, kuhusu kushawishiwa kuingia kwenye
siasa, hakuna mtu aliyenishawishi kugombea ubunge bali ni mimi mwenyewe
niliamua baada ya kuona pia baadhi ya wasanii wenzangu wanagombania kama
nilivyomuona Mr. II Sugu kipindi kile‘-Kingwendu
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ ALICHOKISEMA MCHEKESHAJI KINGWENDU BAADA YA KUSHINDWA UBUNGE KISARAWE.”
Post a Comment