Tuesday, January 26, 2016
MWANAFUNZI WA CHUO CHA IFM AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KUMWINGIZA MTOTO VIDOLE SEHEMU ZA SIRI
Do you like this story?
Mwanafunzi
wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Mussa Msafiri (23), alipandishwa
kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni jana
akituhumiwa kumwingizia vidole sehemu za siri mtoto mwenye umri wa miaka
minne.
Mbele ya Hakimu
Issa Kasailo, Wakili wa Serikali, Matarasa Maharagande, alidai mtuhumiwa
alitenda kosa hilo Januari 7 mwaka huu maeneo ya Sinza alikokuwa
anaishi mwanafunzi huyo.
“Mtuhumiwa
ulitenda kosa hilo wakati ukitambua kwamba ni kinyume cha sheria za Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania,” alidai wakili.
Baada ya
maelezo hayo mtuhumiwa alikana kutenda kosa hilo na upelelezi unaendelea.
Hakimu Kasailo
alisema shitaka hilo linadhaminika hivyo alimtaka mtuhumiwa kuwa na
wadhamini wawili waaminifu watakaoweka saini ya maandishi ya Sh milioni tano
kwa kila mmoja.
Kesi hiyo
imeahirishwa hadi Febuari 27 mwaka huu na mtuhumiwa aliachiwa huru baada ya
kutimiza masharti ya dhamana.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “MWANAFUNZI WA CHUO CHA IFM AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KUMWINGIZA MTOTO VIDOLE SEHEMU ZA SIRI”
Post a Comment