Sunday, January 24, 2016
SAUTHAMPTON, HII NDIYO KAULI MPYA YA VAN GAAL KWA MASHABIKI
Do you like this story?
Boss wa Manchester United Louis van Gaal
amesema yeye pamoja na kikosi chake wanastahili kuzomewa na mashabiki baada ya
kukubali kichapo cha goli 1-0 kutoka kwa Southampton wakiwa kwenye uwanja wao
wa nyumbani Old Trafford.
United imeshindwa kufunga goli kwenye dakika
45 za kipindi cha kwanza kwenye mechi 11 ilizocheza kwenye uwanja wake wa
nyumbani kabla ya jana Charlie Austin kupachika bao la ushindi dakika ya 87.
Man United ipo nafasi ya tano kwenye msimamo
wa ligi kuu England pointi tano nyuma ya Tottenham ambao wako nafasi ya nne na
pointi 10 nyuma ya vinara wa ligi hiyo timu ya Leicester City.
“Wako sahihi kutuzomea. Siwezi kupinga hilo,
niiliuona mchezo”, alisema Van Gaal.
“Kwa mabaya au mazuri bado tunatakiwa kuwa
pamoja”, aliongeza mdachi huyo baada ya kikosi chake kupokea kipigo cha sita
kwenye msimu huu.
United imefanikiwa kuvuna pointi 37 kwenye
michezo yake 23, pointi chache katika historia ya klabu hiyo kwenye ligi ya
England ambazo ni pointi tatu nyuma ukilinganisha na kipindi wakati yupo David
Moyes msimu wa 2013-2014.
“Tunapambana japo tuna idadi kubwa ya
majeruhi”, aliongeza Van Gaal.
Kwenye mchezo wa Jumamosi United ilicheza
bila ya Ashley Young ambaye Van Gaal anasema anakabiliwa na majeruhi ya muda
mrefu. Pia alimpoteza mlinzi wake Matteo Darmian ambaye alitolewa
uwanjani na kupelekwa moja kwa moja hospitali.
Kama beki huyo atakuwa nje ya kikosi, hiyo
inamaanisha kikosi cha United kitakuwa hakina beki mzoefu wa pembeni ambaye
yuko fit huku Luke Shaw akiwa bado anauguza mguu wake uliovunjika September
mwaka jana.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “SAUTHAMPTON, HII NDIYO KAULI MPYA YA VAN GAAL KWA MASHABIKI”
Post a Comment