Sunday, January 24, 2016
SIKIA HII KUTOKA KWA MADEE: ARSENAL IKIFUNGWA NA CHELSEA, GARI YANGU MOJA NAICHOMA MOTO
Do you like this story?
Kama ulikuwa hujui basi leo nakufanya ujue
kwamba mbali na masuala ya music, msanii Madee ni shabiki wa kutupwa wa Arsenal
The Gunners wale watoto wa jiji la London pale England.
Leo Arsenal watakuwa kwenye uwanja wao
kucheza ‘London Derby’ na mahasimu wao wakubwa wa jiji hilo Chelsea.
Kitu kitamu sasa kuelekea kwenye game hiyo ni
pale Madee au wengi hupenda kumwita ‘Rais wa Manzese’ alipoahidi kwamba, endapo
Chelsea itaifunga Arsenal kwenye mchezo wa leo basi yeye ataichoma moto gari
yake moja.
Leo Madee amepost ujumbe huo kwenye account
yake ya instagram unaosomeka: “Tukifungwa leo na Chelsea nachoma moto gari
yangu moja”.
Madee anapata jeuri hiyo kutokana na form
nzuri ya Arsenal waliyonayo msimu huu. The Gunners wameshinda mechi saba na
hawajapoteza mchezo hata mmoja kwenye michezo tisa iliopita ya Premier
League katika dimba la Emirates huku wakiwa wameruhusu magoli manne
katika mechi hizo.
Urejeo wa Mesut Ozil na Alexis Sanchez
unazidi kumpa imani kubwa Madee lakini ikumbukwe pia Eden Hazard ni sehemu ya
kikosi cha Chelsea kwenye game ya leo licha ya nyota huyo kukosa makali msimu
huu.
Data zinaonesha kwamba Chelsea hawajafungwa
na Arsenal kwenye mechi nane zilizopita za Premier League. Chelsea
imeshinda mechi tano na kutoka sare mechi tatu. Arsenal imeifunga Chelsea kwa
mara ya mwisho mwaka 2011 ilipofanikiwa kupata ushindi wa goli 5-3.
Mara ya mwisho Hiddink kukiongoza kikosi cha
Chelsea dhidi ya Arsenal ilikuwa ni mwaka 2009 na akawaachia maumivu Arsenal ya
kipigo kikali kwenye uwanja wa Emirates cha mabao 4-1.
Tusubiri kuona kama Arsenal wataokoa gari la
Madee isichomwe moto au Chelsea watalifanya gari hilo litiwe kibiriti.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “SIKIA HII KUTOKA KWA MADEE: ARSENAL IKIFUNGWA NA CHELSEA, GARI YANGU MOJA NAICHOMA MOTO”
Post a Comment