Tuesday, January 26, 2016
UCHAGUZI WA MBUNGE WA JIMBO LA KIJITOUPELE, ZANZIBAR KUFANYIKA MACHI 20
Do you like this story?
Top of Form
Tume ya Taifa ya Uchaguzi inapenda kuutaarifu Umma
wa Watanzania kuwa Uchaguzi wa Ubunge katika Jimbo la Kijitoupele –
Zanzibar utafanyika mnamo tarehe 20 Machi, 2016.
Uchaguzi wa Mbunge katika Jimbo la Kijitoupele –
Zanzibar ni mojawapo ya Majimbo yaliyoahirisha kufanya Uchaguzi tarehe 25
Oktoba, 2015 kutokana na hitilafu kwenye Karatasi za Kura.
Aidha, Tume inapenda kuwataarifu Wananchi kuwa
Watendaji (Msimamizi wa Uchaguzi na Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi)
walioteuliwa kipindi cha Uchaguzi Mkuu wa 2015 ndio watakaosimamia na kufanya
shughuli za Uchaguzi huo. Uchaguzi huo wa Ubunge katika Jimbo la
Kijitoupele hautakuwa na kampeni na Wagombea walioteuliwa kushiriki
Uchaguzi ulioahirishwa mwezi Oktoba, 2015 ndio watakaoshiriki Uchaguzi
huu.
Vituo vilivyotumika katika Uchaguzi wa mwaka 2015
ndiyo vitakavyotumika. Vituo vitafunguliwa saa 1.00 asubuhi na kufungwa
saa 10.00 jioni. Watakaoruhusiwa Kupiga Kura tarehe 20/3/2016 ni wale
ambao wameandikishwa na majina yao yapo katika Daftari la Kudumu la
Wapiga Kura la Kituo na waje na Kadi ya Mpiga Kura.
Imetolewa na,
Jaji (Mst.) Damian Z. Lubuva
TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI
MWENYEKITI
26/01/2016
Bottom of Form
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “UCHAGUZI WA MBUNGE WA JIMBO LA KIJITOUPELE, ZANZIBAR KUFANYIKA MACHI 20”
Post a Comment