Tuesday, January 26, 2016
WAUZAJI BIDHAA HOLELA SOKO LA BUGULUNI WAPIGWA MARUFUKU.
Do you like this story?
Na Jacquiline Mrisho MAELEZO
Halmashauri ya Manispaa ya Ilala yapiga
marufuku uuzwaji holela wa bidhaa katika soko la Buguruni unaochafua mazingira
ya soko na kuhatarisha afya za walaji.
Hayo yamesemwa leo na Afisa Habari wa
Halmashauri ya Manispaa ya Ilala David Langa wakati akifafanua kuhusu kero ya
wauzaji holela wanaopanga bidhaa chini katika soko la Buguruni.
“Bidhaa zinazopangwa chini katika soko la
Buguruni sio rasmi na hakuna utaratibu unaoruhusu wauzaji kufanya biashara
hiyo, hivyo natoa tahadhari kwa wale wote wenye tabia hiyo kuwa ni marufuku
kufanya biashara ya kupanga bidhaa chini na sio kwa soko la Buguruni tu ila
katika masoko yote yaliyopo katika manispaa yetu” Alisema Langa.
Afisa langa amesema kuwa wapo maaskari
wanaolinda na kuthibiti uuzwaji holela wa bidhaa katika soko hilo ila wauzaji
wamekuwa wakifanya mchezo wa kuwavizia maaskari pindi wanapoondoka ndipo
wanapanga bidhaa zao.
Ameongeza kuwa suala hili limekuwa sugu
katika masoko mengi na njia ya kukabiliana na changamoto hii ni kuongeza askari
wengi watakaokaa muda wote ili waweze kukabiliana na wauzaji holela.
Aidha Halmashauri ya Manispaa ya Ilala kwa
kushirikiana na Maafisa Afya inafatilia kwa karibu masoko yote ili kufatilia
kama wauzaji wanazingatia kanuni za afya kwa kuweka mazingira safi ili kuokoa
afya za walaji.
Uchafu wa mazingira katika masoko ya Jiji la
Dar es Salaam umekithiri na imekuwa ni tatizo sugu lakini Halmashauri ya
Manispaa ya Ilala imejipanga kupambana nalo ili kuondoa uwezekano wa kutokea
kwa magonjwa ya mlipuko kama kipindupindu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ WAUZAJI BIDHAA HOLELA SOKO LA BUGULUNI WAPIGWA MARUFUKU.”
Post a Comment