Thursday, February 25, 2016
NAIBU SPIKA ATOA MSAADA WA MILLIONI TANO(5) SHULE ALIYOSOMA. MBEYA
Do you like this story?
NAIBU spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Tulia Ackson Mwansasu akizungumza na wanafunzi mara Baada ya kufika Shuleni hapo.(Picha na David Nyembe wa Fahari News) |
Maabara ya masomo ya sayansi |
NAIBU spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Tulia Ackson Mwansasu akilitizama Bweni Ambalo alikuwa analala. |
Mbunge wa Jimbo la Songwe, Philip Mulugo akizungumza na Wanafunzi. |
Hili Ndio Bweni Ambalo Mh Tulia Ackson Mwansasu alikuwa anaishi kipindi anasoma. |
Mkuu wa Shule ya wasichana Loleza Mwalimu Emily Fwambo akisoma Taarifa ya shule. |
NAIBU spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania
Tulia Ackson Mwansasu ametoa msaada wa shililingi milioni tano kwa ajili ya
ukarabati wa bweni la Mapinduzi katika Sekondari ya Loleza Mkoani Mbeya.
Amefikia hatua ya kutoa kiasi hicho kwa ajili ya
ukarabati katika bweni ambalo aliishi wakati akisoma elimu ya Sekondari kati ya
mwaka 1991-1994 alipo hitimu kidato cha nne,baada ya kuona halitumiki kutokana
na uchakavu wa dali hali iliyo lazimu uongozi wa shule kulifunga kutokana na
kuhatarisha maisha ya wanafunzi.
Akizungumza mara baada ya kutembelea majengo mbalimbali
ya shule hiyo Mwansasu alisema kuwa licha ya kuwa kuna changamoto nyingi katika
shule lakini amesikitishwa zaidi kuona bweni ambalo aliishi ndani ya miaka
minne likiwa limechakaa na halitimuki tena.
Kutokana na kujionea uchakavu huo Naibu Spika Mwansasu
alisema kuwa ameamua kutoa kiasi hicho cha fedha huku akiahidi kuendelea kusaka
wafadhili mbalimbali ili wawezi kusaidia kuondokana na changamoto mbalimbali
zinazoikabali shule hiyo kongwe hapa nchini ikiwemo ukachakavu wa miuondo mbinu
ya madarasa na mabweni.
Katika hatu nyingine amewasii wanafunzi shule hiyo
kusoma kwa bidii huku wakimtumainia Mungu na kuwataka wanafunzi hao kutambua
kuwa wanategemewa na familia pamoja na taifa kwa jumla hivyo wanapaswa kusoma
kwa kujituma katika masomo yao ili waje kulitumikia taifa kama ambavyo yeye
alijituma na hatimeye leo amepata fursa ya kulitumikia taifa.
Mbali Naibu Spika kutoa kiasi hicho la kiasi hicho
cha fedha lakini pia Mbunge wa Jimbo la Songwe, Philip Mulugo ambaye
aliambatana naye katika zaira hiyo alitoa shilingi milioni moja kwa ajili
ya ukarabati wa miondombinu shule hapo.
Akisoma taarifa ya shule Mkuu wa Shule hiyo Emily Fwambo
alisema kuwa shule hiyo ambayo ilinzishwa mwaka 1948 ikiwa chini ya Wamishinari
wa Kinglikana na baadaye mwaka 1969 kuwa chini ya Serikali imekuwa ikifanya
vizuri katika mitahani ya kidato cha Sita kitaifa kwani matokeoa ya mwaka jana
kidato cha sita wanafunzi walifauli kwa asilimia mia moja.
Amesema kuwa licha ya
kuwa na mafanikio hayo kitaalumu lakini shule hiyo imeikuwa ikikabiliwa
na changamoto nyingi ikiwemo ukosefu wa uzio kiasi kinacho palekea wanafunzi
kuruka na kwenda kuzurula mitaani.
Aidha Mkuu wa huyo amesema mbali na uzio lakini pia shule
hiyo ambayo ina kidato cha tano na sita pekee inakabiliwa changamoto ya bwalo
la chakula hali inayo walamizimu wanafunzi kula chakula wakiwa wamesimama na
wengine wakilazimika kukaa nje.
‘Mheshimiwa Naibu Spika kwanza nishukuru kwa ujio wako
lakini pamoja mafanikio tuliyo nayo kitaaluma lakini tuna changamoto ikiwemo
uhaba wa madarasa, uzio na uchakavu wa mabweni, kubwa ni hili na bwalo la
chakula kwani awali lilijengwa kwa ajili ya kuhudumia wanafaunzi 300 lakini mpaka
sasa tunawafunzi 831 hivyo tunahitaji msaada wako wa hali na mali ili
kuondokana na changamoto hizi’ alisema Fwambo mkuu wa shule hiyo ambaye pia ni
muhitimu wa kidato cha nne mwaka 1986
Aliongeza kuwa kwa upande wa mabweni shule hiyo inayo 18
lakini ni mabweni 16 ndiyo yanayo tumika na mawili hayatumiki likiwemo bweni la
Mapinduzi ambalo aliishi akiwa anasoma.
Aliongeza kuwa kutokana na watalaamu kufanya upembuzi
shule hiyo inahitaji mabati 393 geji 28 ili kukamilisha majengo yote.
mwisho
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “NAIBU SPIKA ATOA MSAADA WA MILLIONI TANO(5) SHULE ALIYOSOMA. MBEYA”
Post a Comment