Friday, February 19, 2016

RAIS MUSEVENI ANAONGOZA MATOKEO YA AWALI. UGANDA





MATOKEO ya awali ya Uchaguzi Mkuu nchini Uganda yaliyotangazwa na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi (EC),
Eng. Badru Kiggundu leo asubuhi yanaonyesha Rais Museveni anaongoza kwa kupata kura 1,362,961 sawa na
asilimia 61.75 huku mpinzani wake wa karibu Kizza Besigye akifuatia kwa kupata kura 738,628 sawa na
asilimia 33.47 na aliyewahi kuwa Waziri Mkuu Amama Mbabazi mpaka sasa yeye ana kura 41,291 sawa na
asilimia 1.87.

Matokeo hayo ni kutoka katika vituo 6,448 kati ya 28,010 vilivyotumika kupigia kura.
Jumla ya watu 15,277,198 walijiandikisha kwa ajili ya uchaguzi wa mwaka huu.

0 Responses to “ RAIS MUSEVENI ANAONGOZA MATOKEO YA AWALI. UGANDA”

Post a Comment

More to Read