Friday, February 19, 2016
TCU YAFUTA VYUO VISHIRIKISHI VYA MTAKATIFU JOSEPH
Do you like this story?
Tume
ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) imeamua kufuta kibali
kilichoanzisha vyuo vikuu viwili vishiriki vya Mtakatifu Joseph ambavyo ni Chuo
Kikuu kishiriki cha Sayansi ya Kilimo na Teknolojia (SJUCAST) na Chuo Kikuu
kishiriki cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (SJUIT) vilivyopo Songea.
Akizungumza na waandishi wa habari leo katika ofisi za Tume hiyo, Katibu
Mtendaji wa Tu
me ya Vyuo Vikuu Tanzania Prof Yunus Mgaya amesema kutokana na mapungufu
yaliyobainishwa na Tume ambayo ni matatizo ya ubora wa elimu na ukiukwaji wa
Sheria za uendeshaji wa Chuo Kikuu kama ulivyobainishwa na Sheria ya Vyuo Vikuu
hii imepelekea Tume kuchukua hatua ya kufuta usajili wa vyuo hivyo.
“ kutokana na yaliyobainishwa hapo awali tunapenda kutaarifu umma kwamba
,Tume imejiridhisha kuwa hivi vyuo vikuu vishiriki viwili havitoi elimu ya Chuo
kikuu ya viwango stahiki na ukizingatia wanafunzi katika Vyuo hivi ndio
waathirika wakubwa wa matatizo yaliyopo”Alisema Prof Mgaya.
“Napenda kufafanua kwamba Vyuo vikuu vishiriki tuliyovifutia usajili ni
tawi la Songea na Vyuo vingine vishiriki vya Mtakatifu Joseph vilivyopo Dar es
Salaam na Arusha vitaendelea kufanya kazi kama kawaida”Alisema Prof Mgaya.
Prof Yunus Mgaya amesema wanafunzi wote wanaosoma katika vyuo vishiriki
vilivyofutwa usajili wanaarifiwa kuwa watahamishiwa kwenye vyuo vikuu vingine
vinavyofundisha programu za masomo zinazofanana na masomo wanayosoma hivi sasa
chini ya utaratibu uliopangwa.
Amevitaja vyuo ambavyo watapelekwa wanafunzi walipo katika vyuo vishiriki
vilivyofutwa usajili kuwa ni Chuo Kikuu cha kilimo Sokoine (SUA), Chuo Kikuu
cha Dodoma (UDOM),Chuo Kikuu cha Kikatoliki cha Mwenge(MWECAU) na Chuo
Kikuu cha Kikatoliki cha Ruaha(RUCU).
Amesisitiza kuwa orodha ya majina ya wanafunzi na vyuo watavyohamishiwa
yatawekwa kwenye tovuti ya Tume hivi karibuni na wale wote wanaonufaika na
Mikopo toka Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, mikopo yao
itahamishiwa katika vyuo watakavyokuwa wamehamishiwa.
Vyuo vikuu vyote chini vinakumbushwa kufata Sheria na kuzingatia utoaji
wa elimu inayokidhi viwango vya ubora vinavyokubalika kitaifa na kimataifa,
hivyo Tume haitasita kuchukua hatua stahiki kwa chuo kikuu chochote kitakachobainika
kutoa elimu isiyokidhi viwango vya ubora kwa kisingizio cha aina yoyote.
Imeandaliwa na Nyakongo Manyama MAELEZO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ TCU YAFUTA VYUO VISHIRIKISHI VYA MTAKATIFU JOSEPH”
Post a Comment