Saturday, March 12, 2016

ANGALIA REFA WA CHINA ALICHOMFANYIA DEMBA BA (Video)




Shanghai SIPG na Shanghai Shenhua walipambana kwenye mchezo wa ligi ya China jana Ijumaa huku mechi hiyo ikiwa na jumla ya washambuliaji watatu kutoka Afrika; Demba Ba, Obafemi Martins pamoja na Asamoah Gyan.

Akiwa amekosa penati katika kipindi cha kwanza, mambo yaliendelea kuwa magumu kwa mshambuliaji wa zamani wa Chelsea na Newcastle United Demba Ba.

Akiwa anajiandaa kuruka ili kupiga mpira kwa kichwa mapema kipindi cha kwanza, Ba alijikuta anatupwa chini na mwamuzi wa pambano hilo ambaye alikuwa anakimbia na kukaa kwenye nafasi ambayo alikuwepo Ba.

Cheki video hapa ushuhudie tukio zima lilivyokuwa

0 Responses to “ANGALIA REFA WA CHINA ALICHOMFANYIA DEMBA BA (Video)”

Post a Comment

More to Read