Monday, March 14, 2016
CHANETA WAPIGA MSASA WALIMU 100 MBEYA.
Do you like this story?
Mwenyekiti wa Vijana Mkoa wa Mbeya (Uvccm )Amani Kajuna ambae ndio Mgeni Rasmi akikabidhi Cheti kwa mmoja wa washiriki wa semina hiyo..(Picha na David Nyembe wa Fahari News) |
Washiriki wakiwa makini kumsikiliza Mgeni Rasmi..(Picha na David Nyembe wa Fahari News) |
Mwenyekiti wa Vijana Mkoa wa Mbeya (Uvccm )Amani Kajuna ambae ndio Mgeni Rasmi akikabidhi Cheti kwa mmoja wa washiriki wa semina hiyo..(Picha na David Nyembe wa Fahari News) |
Mwenyekiti wa Vijana Mkoa wa Mbeya (Uvccm )Amani Kajuna ambae ndio Mgeni Rasmi akikabidhi Cheti kwa mmoja wa washiriki wa semina hiyo.(Picha na David Nyembe wa Fahari News) |
Mwenyekiti wa Vijana Mkoa wa Mbeya (Uvccm )Amani Kajuna ambae ndio Mgeni Rasmi akikabidhi Cheti kwa mmoja wa washiriki wa semina hiyo..(Picha na David Nyembe wa Fahari News) |
Ulifika muda wa keselebuka mara baada ya kupewa Vyeti na Mgeni Rasmi Mwenyekiti wa Vijana Mkoa wa Mbeya (Uvccm )Amani Kajuna.(Picha na David Nyembe wa Fahari News) |
MWENYEKITI wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (Uv-CCM),
Mkoa wa Mbeya, Aman Kajuna, amewataka walimu waliofanikiwa kupata mafunzo
ya taaluma ya michezo kuwa chachu ya kuibua vipaji na kustawisha michezo hapa
nchni.
Kajuna alitoa wito huo juzi wakati akifunga mafunzo ya wiki mbili
kwa walimu wa mchezo wa mpira wa Pete kwa walimu zaidi ya 100 wa shule za
msingi na sekondari, Mkoa wa Mbeya.
Amesema ili lengo la mafunzo hayo liendane na uhalisia, ni vizuri
walimu hao waliopatiwa mafunzo kwa kushirikiana na Chama cha mchezo huo
(Chaneta) kuhakikisha wanaibua vipaji kadili vinavyopatikana ili kustawisha
mchezo huo.
Hata hivyo, aliwataka viongozi wanaoratibu walimu kushiriki
mafunzo mbalimbali ya michezo kuteuwa walimu ambao kweli wanahusika na michezo,
badala ya kupeleka walimu wasiokuwa na sifa ya kujihusisha na michezo.
Awali akitoa taarifa ya mafunzo hayo, Ofisa michezo wa Jiji la
Mbeya, Joyce Mwakifamba, aliwataka walimu waliobahatika kupata mafunzo hayo kutumia
fursa hiyo vizuri na kuwa chachu ya kuleta mabadiliko chanya katika ufundishaji
wa mchezo wa mpira wa netiboli kwa watoto.
‘’Napenda kuwakumbusha kuwa mmechaguliwa miongoni mwa walimu walio
wengi kushiriki mafunzo haya hivyo, itumieni fursa mliyoipata vizuri na hata
maporejea katika vituo vyenu vya kazi mkaache mtindo wa kufanya kazi kwa mazoea
bali kujituma na kutanguliza uzalendo” alisema.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Cheneta Mkoa wa Mbeya, Shizya
Mwakatundu alisema mafunzo hayo ya awali ya ualimu wa mchezo wa pete yatakuwa
endelevu kwa lengo la kukuza mchezo huo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “CHANETA WAPIGA MSASA WALIMU 100 MBEYA.”
Post a Comment