Sunday, March 6, 2016
RONALDO APIGA NNE, MADRID IKISHINDA GOLI 7 - 1 DHIDI YA CELTA VIGO
Do you like this story?
Staa wa Real Madrid na timu ya taifa ya Ureno, Cristiano Ronaldo
ameisaidia timu yake ya Real Madrid kuibuka na ushindi mnono wa goli saba kwa
moja walipokuwa wakipambana na Celta Vigo katika mchezo wa Ligi Kuu ya
Hispania.
Ronaldo alifunga magoli hayo katika dakika ya 50, 58, 65 na 76 na hivyo
kufikisha hat trick ya 36 katika historia yake ya maisha ya soka.
Magoli mengine ya Real Madrid yalifunga na Pepe dk. 41, James Rodriguez
dk.78 na Gareth Bale dakika ya 81 na goli pekee la Celta Vigo likifungwa na
Iago Aspas dk.62.
Baada ya ushindi huo Madrid imefikisha alama 60 ikiwa nyuma kwa nafasi
moja na Atletico Madrid iliyo katika nafasi ya pili.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “RONALDO APIGA NNE, MADRID IKISHINDA GOLI 7 - 1 DHIDI YA CELTA VIGO”
Post a Comment