Thursday, March 10, 2016
WAANGALIZI WA NDANI WA UCHAGUZI (CEMOTWAKATAA KUSHIRIKI KATIKA UCHAGUZI WA MARUDIO ZANZIBAR
Do you like this story?
Muungano wa Waangalizi wa Ndani wa
Uchaguzi (Cemot) umesema hautashiriki katika uangalizi wa uchaguzi wa marudio
Zanzibar utakaofanyika Machi 20 mwaka huu kutokana na kukabiliwa na ukata.
Cemot ni umoja
wa taasisi za waangalizi wa ndani wa uchaguzi inayohusisha Kamati ya Uangalizi
wa Uchaguzi (Temco) na Muungano wa taasisi zisizo za kiraia za kusimamia
uchaguzi (Tacceo) ambazo zilitumia waangalizi katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba
25, mwaka jana.
Akizungumza na
waandishi wa habari Arusha katika warsha ya mrejesho wa taarifa ya waangalizi
wa ndani wa Uchaguzi Mkuu, Mwenyekiti mwenza wa Cemot, Martina Kabisama alisema
fedha zote zilitumika katika uchaguzi uliopita.
“Kwenda
kuangalia uchaguzi ni jambo linalohitaji rasilimali, hivyo hatutakwenda
Zanzibar katika uchaguzi wa marejeo kwa kuwa tulikuwa hatujaandaa andiko la
kupata fedha za uchaguzi huo,” alisema.
Kabisama
alisema Cemot ilikuwa na waangalizi wa muda mfupi 9,400 na wengine 350
waliotoka Tacceo na Temco.
Mwangalizi wa
ndani wa Uchaguzi Mkuu kwa Tanzania Bara na Visiwani, Dk Alexander Makulilo
alisema Cemot ilifanya kazi kubwa katika uangalizi na imeandaliwa taarifa
inayoonyesha mahitaji ya maboresho katika chaguzi zijazo.
Dk Makulilo
ambaye anaongoza timu ya uandishi wa taarifa ya Cemot, alisema uchaguzi wa
Zanzibar uliopita ulikwenda vizuri licha ya kuwapo dosari kidogo sawa na
Tanzania Bara.
Alisema Tume ya
Uchaguzi Zanzibar (ZEC) na mashirika yasiyo ya kiserikali, walifanya kazi ya
kutoa elimu ya wapigakura, tofauti na Tanzania Bara.
Pia alisema
visiwani humo polisi walitekeleza vizuri wajibu wao tofauti na Tanzania Bara.
Dk Makulilo
alisema asilimia 87 ya waangalizi wa Zanzibar walieleza polisi walifanya kazi
nzuri kwa asilimia 65 kutokana na kusimamia vema uchaguzi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “WAANGALIZI WA NDANI WA UCHAGUZI (CEMOTWAKATAA KUSHIRIKI KATIKA UCHAGUZI WA MARUDIO ZANZIBAR”
Post a Comment