Friday, March 4, 2016
WAZIRI NAPE APIGA STOP TIKETI ZA TFF,ATAKA MALIPO YA KIELEKRONIKI UWANJA WA TAIFA.
Do you like this story?
Waziri wa Habari, Utamaduni, Wasanii na Michezo, Mh. Nape Nnauye ametoa
agizo rasmi juu ya matumizi ya tiketi za Kielekroniki michezoni kwa kulitaka
Shirikisho la Soka la Tanzania (TFF) kuakikisha linatumia tiketi hizo kuanzia
Machi 9.2016 na kuachana na tiketi za kawaida huku akibainisha kuwa wataendelea
kulifuatilia suala hilo kwa ukaribu na hatua zaidi ilikuziba mianya ya
udanganyifu.
Nape amebainishahayo muda huu wakati anazungumza na vyombo vya habari
kuelezea suala la Michezo hapa nchini ikiwemo suala hilo la mfumo wa malipo kwa
njia ya Kielekroniki ambapo awali Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alitoa agizo la
matumizi ya mfumo huo.
Akielezea suala hilo, amesema litaondoa ‘figisufigsu’ za mara kwa
mara ambazo watu wamekuwa wakilalamikia mapato ikiwemo hayo ya Uwanja wa Taifa.
“Baada ya Machi 8 mwaka huu. Mechi zote zitakazochezwa uwanja wa Taifa,
tiketi zote zitatumika ni zile za kieletroniki. Hii ni mara baada ya michezo
yote mitatu iliyobaki ambayo TFF wanamalizia tiketi zao ambazo wamebazibakisha
na zinaisha Machi 8. Safari hii tutafuatilia na kukagua wenyewe. Hatutakubali
kuendelea kuvumilia hujuma katika hili.” Ameeleza Nape katika mkutano huo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ WAZIRI NAPE APIGA STOP TIKETI ZA TFF,ATAKA MALIPO YA KIELEKRONIKI UWANJA WA TAIFA.”
Post a Comment