Wednesday, August 24, 2016
KOFIA YA MZEE AKILIMALI YARUDISHWA
Do you like this story?
Kofia ya Katibu
wa Baraza la wazee katika klabu ya Yanga Mzee Ibrahim Akilimali hatimaye
imepatikana baada ya alieichukua kuirudisha polisi.
Mzee Akilimali
ambaye amejizolea umaarufu mkubwa kipindi cha hivi karibuni baada ya yeye
kupinga wazo la Mwenyekiti wa Yanga Yusuph Manji kutaka kuichukua timu ya Yanga
kwa mkopo, alipoteza kofia yake wakati alipomtembelea mzee mwenzake Hashim
Mhika, Mtoni. Kofia yake ilipotea wakati alipomfuata mzee mwenzake katika mkeka
na kuiacha kofia yake chini na aliporudi watoto wa mjini tayari walikuwa
wameshaiichukua.
Alipoulizwa kuhusiana
na kupotea kwa kofia yake Mzee Akilimali alisema kuwa kwa vyovyote vile lazima
alieichukua atairudisha na kweli hatimaye alieichukua ameirudisha na tayari
mzee Akilimali amethibitisha kuwa kofia yake imepatikana.
Mzee Akilimali
alijijengea umaarufu kutokana na staili yake aliyoitumia wakati baadhi ya wazee
walipotofautiana na uongozi wa Lloyd Nchunga. Mzee Akilimali aliitisha mkutano
na waandishi wa habari na kuelezea machungu yake kisha akasema wao kama wazee
wanavua kofia (kasha wakazivua na kuziweka mezani). Kilichofuata ni Yanga
kufungwa tano na Simba, matokeo yaliyoambatana na Nchunga kubwaga manyanga.
Source #TanzaniaDaima
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


.gif)


0 Responses to “KOFIA YA MZEE AKILIMALI YARUDISHWA ”
Post a Comment