Monday, August 22, 2016
MAAMBUKIZI MAPYA YA VIRUSI VYA UKIMWI (VVU) YAPUNGUA
Do you like this story?
Serikali
imefanikiwa kupunguza vifo vya akina mama na watoto pamoja na maambukizi mapya
ya virusi vya ukimwi (VVU)katika kipindi cha miaka kumi kuanzia mwaka 2005 hadi
2015.
Hayo yamesemwa
leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu
wakati akitoa ripoti ya utekelezaji wa sera ya afya ya mwaka 2005/2015 jijini
Dar es Salaam.
Kuhusu
vifo vya akina mama na watoto, Ummy amesema kuwa vifo vya watoto wanaozaliwa
vimepungua kutoka vifo 112 katika kila vizazi hai 1,000 kwa mwaka 2005 hadi
kufikia 54 katika kila vizazi hai 1,000 kwa mwaka 2010 .
“Mwaka
2005 idadi ya vifo vilivyotokea ni 578 katika vizazi hai laki moja, lakini kwa
mwaka 2012 vimepungua hadi kufikia 432 katika vizazi hai 100,000.” amesema.
Amesema
ingawa serikali imefanikiwa kuvipunguza vifo hivyo, atahakikisha anapambana na
vifo vya akina mama na watoto.
Kuhusu
maambukizi mapya ya VVU, amesema yamepungua kutoka asilimia 7 kwa mwaka 2004
hadi asilimia 5 kwa mwaka 2012/2015.
“Maambukizi
mapya ya VVU yamepungua ambapo sasa kati ya watu 100, watu 5 wanamaambukizi
mapya ya VVU, ” amesema.
Amesema
serikali imefanikiwa kutoa huduma za afya kwa walionaupungufu wa kinga mwilini
(Ukimwi) ikiwa ni pamoja na kutoa dawa za kupunguza Makali (ARV)
“Awali
wagonjwa 16,199 nchi nzima ndiyo walikuwa wanapata vidonge vya kupunguza makali
lakini sasa zaidi ya wagonjwa laki saba nchi nzima huipata huduma hiyo, ”
amesema.
Ameongeza
“Katika vituo vya kutoa huduma za wagonjwa wa ukimwi wagonjwa wamepungua jambo
linaloashiria kuwa wagonjwa wapya wamepungua.” amesema.
Amesema
hivi sasa serikali imeandaa sera inayofahamika kama ‘Pima na Tibu’, kwa lengo
la kila mtanzania kupima VVU na watakaobainika na maambukizi wataanzishwa dozi
ya kupunguza makali papohapo.
Aidha,
Ummy amesema kuwa katika kipindi cha miaka kumi ya utekelezaji wa sera hiyo
serikali imefanikiwa kuongeza vituo vya afya kutoka 5,172 na sasa kunavituo
zaidi ya 7,000.
“Changamoto
iliyojitokeza ni kwamba licha ya kuongeza vituo vya afya bado kunachangamoto ya
miundombinu. Upungufu wa watumishi wa afya hususan katika mikoa ya kanda ya
ziwa,” amesema.
Na Regina
Mkonde
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


.gif)


0 Responses to “ MAAMBUKIZI MAPYA YA VIRUSI VYA UKIMWI (VVU) YAPUNGUA”
Post a Comment