Monday, August 22, 2016
MKUU WA WILAYA YA IRINGA AWASHIKISHA ADABU WALINZI WA HOSPITALI YA RUFAA YA IRINGA
Do you like this story?
Maneno
kutoka kwa Mkuu wa wilaya ya Iringa "jana saa 3 na dakika 25 Usiku
nilipokea wakina mama 3 wakiwa wanatetemeka kwa baridi, wakilalamika kumwagiwa
maji walipokuwa wamekaa kwenye eneo la kusubiria wagonjwa walio lazwa hasa kwa
wale walio toka mbali.
Maji
hayo yalimwagwa na walinzi wa kampuni ya Amazon ambao ndio wamepewa kandarasi
ya ulinzi hospitali ya Rufaa ya Iringa.
Nilifika
hospitali kujionea mwenyewe hali halisi, baadae nikapata taarifa kuwa jana yake
Mlinzi alimpiga mzee aliyekuwa ameleta chakula hospitali na kumwaga kwa mateke.
Niliamuru
mlinzi huyo na mwenzake wakamatwe pia mwenye kampuni afike kituo cha polisi
haraka iwezekanavyo.
Hali
hii imeudhi sana hasa ukiona jinsi wakina mama walivyo nyanyasika wengine
vyombo vyao na chakula kuroweshwa maji."
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


.gif)






0 Responses to “ MKUU WA WILAYA YA IRINGA AWASHIKISHA ADABU WALINZI WA HOSPITALI YA RUFAA YA IRINGA ”
Post a Comment