Monday, August 22, 2016

MSOMALI FEYISA LILESA ASHINDA MEDALI YA SILVER LAKINI ANAOGOPA KURUDI KWAO




Mwanariadha kutoka Taifa la Ethiopia Feyisa Lilesa amefanikiwa kushinda medali ya Shaba katika mbio za marathon kwenye michuano ya Olimpiki Rio Brazili lakini anaogopa kurudi nchini kwao kwa hofu ya kuuliwa au kufungwa jela.

Hi imekuja baada ya Lilesa kuonesha alama ya msalaba kwa kutumia mikono yake wakati akimalizia kuvuka mstari wa mwisho, ishara hii hutumika na waandamanaji wanaopinga serikali iliopo madarakani nchini Ethiopia.

Akiongea na vyombo vya habari baada ya tukio hili alisema “nilionesha vile katika kusapoti familia yangu na ndugu zangu ambao wamefungwa jela”




“Kama nikiamua kurudi nyumbani wataniua, na kama sio kuniua basi watanifunga au kunizuia pindi nitakapotua uwanja wa ndege, hivyo nimeamua kwenda kwenye nchi nyingine kwa sasa” aliongeza Lilesa.

Katika maelezo yake aliendelea kusisistiza kuwa serikali iliyopo madarakani ni serikali mbaya na onevu ambayo pindi mataifa ya Marekani, Uingereza na Ufaranza wanapowapa sapoti basi wao hutumia fedha hizo kwenye kununulia silaha ambazo huzitumia kuulia watu.

0 Responses to “MSOMALI FEYISA LILESA ASHINDA MEDALI YA SILVER LAKINI ANAOGOPA KURUDI KWAO ”

Post a Comment

More to Read