Monday, August 29, 2016
YAFAHAMU MATUKIO MANNE MAKUBWA SEPTEMBER MOSI
Do you like this story?
Septemba
mosi mwaka huu inatarajiwa kuwa siku ya kipekee kutokana na nchi yetu kuwa na
matukio makubwa manne ya kihistoria ambayo yamekuwa yakisubiriwa kwa hamu na
watanzania wengi nchini.
Matukio
hayo ni :-
1. Tukio la kupatwa kwa
jua tukio hili ni la kihistoria likijirudia baada ya miaka 36 iliyopita,
Tanzania ni miongoni mwa nchi za Afrika ambazo zitaweza kushuhudia tukio hillo
vizuri katika mji wa Lujewa Wilayani Mbarare mkoani Mbeya na maeneo mengine
kama Katavi,Ruvuma na Masasi.
2. Maadhimisho ya Miaka
52 ya Jeshi la Wananchi (JWTZ)
Jeshi la
wananchi linatarajiwa kuadhimisha miaka 52 tangu kuanzishwa kwake mwaka 1964
kwa kufanya zoezi la kufanya usafi
katika maeneo tofauti.
Mbali na
usafi madaktari wa JWTZ watatoa huduma tiba bure kama upimaji wa virusi vya
Ukimwi, Kisukari na shinikizo la damu na kushiriki katika michezo mbalimbali na
Taasisi nyingine.
3. Maandamano ya Chadema (UKUTA)
Chama cha
demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimepanga kufanya maandamano nchi nzima
kupinga kauli ya Mh Rais Dkt. John Magufuli ya kufungia mikutano yote ya vyama
vya siasa nchini
Maandamano
hayo yanaleta sura nyingine kwani jeshi la Polisi Nchini limejiandaa kukabiliana
na kundi lolote litakalokuwa likifanya maandamano siku hiyo kwani watakua wamekiuka
kauli ya Mh Rais, tangu chama cha CHADEMA kutangaza siku hiyo jeshi laPolisi
limeonekana katika mikoa mbalimbali kufanya mazoezi ambayo ni sehemu ya kawaida
ya jeshi hilo huku baadhi ya watu wakiielezea kuwa ni sehemu ya kujiandaa na
maandamano hayo yaliyopewa jina maarufu UKUTA
4. Waziri Mkuu kuhamia rasmi Dodoma
Septemba
mosi ni siku ambayo Waziri Mkuu Kassim Majaliwa anatarajiwa kuhamishia ofisi
yake Rasmi Mkoani Dodoma kwa kutekeleza agizo la Rais Dkt John Pombe Magufuli
la kutaka Serikali ihamie katika mji ambao ndio Makao Makuu ya Nchi (Dodoma)
Majaliwa
atakuwa ndio Kiongozi wa kwanza kuhamia Dodoma huku baadhi ya mawaziri wengine kuahidi kutekeleza agizo hilo mwezi Septemba
mwaka huu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


.gif)

0 Responses to “YAFAHAMU MATUKIO MANNE MAKUBWA SEPTEMBER MOSI”
Post a Comment