Saturday, August 20, 2016

SIMBA YAANZA VIZURI LIGI KUU, YAICHAPA 3-1 NDANDA.








Simba Ikicheza mchezo wake wa kwanza kwenye ligi kuu Tanzania bara,Kikosi cha Simba leo kimeuanza vema msimu huu 2016/17 baada ya kamaliza mchezo wake na Ndanda Fc Kwa mabao 3 - 1.

Mchezo uliokuwa mkali na wakuvutia ambapo pande zote mbili zilionekana zenye hamu ya kuibuka na ushindi wa mchezo wa leo. Kipindi cha kwanza kilimalizika Kwa timu zote mbili kufungana 1 - 1 ambapo goli la Simba likifungwa na mshambuliji wake wa kimataifa Laudit Mavugo wakati Ndanda goli lao liliwekwa kimyani na  Omary Mponda.

Katika Kipindi cha pili Simba kuifanya mabadiliko ambayo yaliweza kuisaidia kuongeza goli la pili likifungwa na mchezaji wake wa kimataifa Blagnon ambaye aliingia akabadilishana na Ibrahim Ajib. Ndani ya dakika za lala salama Simba ilipata goli la 3 kupitia mchezaji wake Kichuya ambapo mpaka kipenga cha mwisho kinapigwa Simba 3 - 1 Ndanda Fc



(Picha zote na Robert wa Fahari News)

0 Responses to “SIMBA YAANZA VIZURI LIGI KUU, YAICHAPA 3-1 NDANDA.”

Post a Comment

More to Read