Tuesday, September 13, 2016
KILIMANJARO QUEENS WAANZA MASHINDANO KWA KUTOA KICHAPO KIKALI
Do you like this story?
Timu ya Taifa
ya wanawake Kilimanjaro Queens imewashushia kichapo cha goli 3-2 timu ya Rwanda
Katika mchezo wao wa kwanza wa mashindano ya Chalenji, mchezo uliopigwa jana huko Jinja Uganda
Kilimanjaro
Queens ndio walikuwa wa kwanza kuziona nyavu za wapinzani wao mnamo dakika ya
11 ya mchezo kupitia kwa Asha Rashidi na
bao la pili kuwekwa wavuni na Stumai Abdallah katika dakika ya 28
Makosa yaliyo
fanyika na mabeki wa Kilimanjaro Queens
katika kipindi cha pili yaligharimu timu yao baada ya kujifunga wenyewe
kupitia kwa Amina Ally na kufanya Rwanda kupata mabao 2-2
Mnamo dakika
ya 65 ya kipindi cha pili Asha Rashidi alizichungulia tena nyavu za
Rwanda na kuandika goli la 3 Kilimanjaro
Queens goli lililowabana mbavu Rwanda na kukubali matokeo hayo
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


.gif)

0 Responses to “KILIMANJARO QUEENS WAANZA MASHINDANO KWA KUTOA KICHAPO KIKALI”
Post a Comment