Monday, September 12, 2016
WATU WATATU WAMEKAMATWA KWA KUIBA NG"OMBE WA RAIS
Do you like this story?
KAMPALA:
Wanaume watatu wanaotuhumiwa kuiba ng’ombe katika shamba binafsi la Rais Yoweri
Museveni wa Uganda wamekamatwa. Mmoja kati ya watuhumiwa hao anafanya kazi
katika shamba la Rais Museveni, na yeye pamoja na wenzake walikuwa wakiwapeleka
ng’ombe hao katika mnada ili kuwauza.
Watuhumiwa hao walikiri kuwa wamekuwa wakiiba ng’ombe kabla ya
kukamatwa, alisema Afisa wa Polisi Doreen Kachwo.
Aidha, alieleza kuwa uchunguzi unaendelea na utakapokamilika
watuhumiwa wote watapelekwa mahakamani.
Rais Museveni ambaye ameiongoza Uganda kwa miongo mitatu sasa
hupenda kutembelea eneo hilo mara kadhaa awapo na wageni kutoka mataifa
mbalimbali.
![]() |
| Rais Yoweri Museveni wa Uganda akiwa na Rais Paul Kagame wa Rwanda katika shamba analofugia ng’ombe. |
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


.gif)



0 Responses to “WATU WATATU WAMEKAMATWA KWA KUIBA NG"OMBE WA RAIS”
Post a Comment