Friday, December 16, 2016
BWANAHARUSI AINGIA MITINI MUDA MCHACHE KABLA YA NDOA JIJINI MBEYA
Do you like this story?
Samwel Mwakalobo Bwanaharusi ambaye ameingia mitini muda mchache kabla kuingia kanisani kufunga ndoa katika kanisa la K.K.K.T Isanga jijini Mbeya. |
Mwisho
wa mwaka 2016 huenda ukamaliza na kituko cha aina yake katika Mitaa ya Isanga Jijini Mbeya Mkoa wa
Mbeya mara baada ya bwanaharusi kuingia
mitini masaa machache kabla ya kufunga ndoa.
Tukio
hilo la aina yake limeibua maswali mengi kwa ndugu jamaa na marafiki ambao
walikuwa tayari kwa maandalizi ya kuhudhuria harusi hiyo kuanzia kanisani hadi
ukumbini.
Imeelezwa
kuwa mipango yote ya harusi ilifanyika kwa pande zote mbili kushiriki kwa kufuata taratibu zote zinazotakiwa
kufuatwa hadi hatua ya mwisho ya kuingia kanisani ambapo kama kawaida ndugu
jamaa wote walihudhuria kanisani kwa lengo la kushuhudia tukio hilo .
Tukio
rasmi lilianza majira ya saa 7 mchana katika kanisa la K.K.K.T Usharika wa Isanga jijini Mbeya Desemba 16 ambapo kama kawaida Bibi harusi akiongozana
na wapambe wake akifuata na msafara wa magari zaidi ya manne akitokea Saloon na kuingia kanisani hapo.
Baada
ya bibi harusi kuingia kanisani tayari kwa kufunga ndoa hiyo taarifa zilianza kuenea kuwa bwanaharusi
hayupo kanisani hapo na hajulikani mahali alipo.
Kadri
muda ulivyozidi kwenda bila bwana harusi kufika kanisani hapo baadhi ya Ndugu,
jamaa na watu waliohudhuria harusi hiyo
walianza kuhoji ambapo kwa muda huo yalipita zaidi ya masaa 4 bila chochote
kuendelea kanisani hapo.
Kadi ya mwaliko kwa ajili ya sherehe |
Bibi harusi Given Mgaya Mkazi wa Isanga jijini Mbeya |
Akielezea
mkasa huo Mchungaji kanisa la K.K.K.T Usharika wa Isanga Ndugu Andagile
Mwakijungu amesema jambo hilo amelipokea kwa masikitiko makubwa kwani
halijawahi tokea toka ameanza kutoa huduma kanisani hapo.
Amesema
taratibu zote za kufungwa ndoa hiyo zilifanyika na Jana Desemba 15 majira
ya saa 10 jioni wahusika wote Samwel Mwakalobo ambaye ni
bwana harusi na Given Mgaya ambaye ni bibi harusi walifika nyumbani kwa baba
mchungaji na kuafikiana kuwa harusi hiyo ifanyike leo majira ya saa 7
mchana Desemba 16 kanisani hapo hivyo kitendo cha bwanahurusi kutofika bila
sababu yoyote yeye mwenyewe imestua hasa kutokana na mipango ilivyokuwa
imepangwa vizuri .
Amesema
jambo hilo limetokea wakati yeye akiendelea kufanya maandalizi ya
kusubiri kutoa huduma ya kufunga ndoa kati ya wawili hao .
Amesema
wakati akiendelea kusubiri ili kufungisha ndoa hiyo walitokea ndugu upande wa
mume ambao waliomba msaada kwa mchungaji ili awasaidie kumtafuta kijana wao
ambaye ni bwanaharusi kwa njia yoyote ili kufaham chanzo kilichopelekea
kushindwa kufika kanisani hapo bila kutoa sababu zozote.
Amesema
alichukua jukumu la kumtafuta kijana huyo ambapo alifanikiwa kumpata na
kuzungumza nae ambapo kijana huyo alimueleza kuwa anatatizo na baadae
angefika kwa mchungaji ili kumueleza.
“Baada
ya wazazi kufika na kunieleza kuwa nisaidie kumtafuta kijana wao nilichukua
jukumu hilo na nilifanya hivyo na nilifanikiwa kumpata lakini alicho nijibu
nikuwa mchungaji ninatatizo hivyo nitafika ofisini kwako kukueleza na kwa sasa
nipo njiani nikitokea Tunduma ”Amesema
Mchungaji
amesema kuwa wakati wanaendelea na majadiliano ya nini kifanyike ghafla
walipata ujumbe kutoka kwa mpambe wa bwanaharusi ambao ulitumwa na bwanahaurusi
mwenyewe ukieleza kuwa asingeweza kufika ili kufunga ndoa hiyo bila
kueleza sababu yoyote.
Kufuatia
tukio la bwanaharusi kuingia mitini huku jitihada za kumpata kushindiana
Mchungaji huyo aliamua kusitisha zoezi la ufungaji wa ndoa hiyo.
“Nimejaribu
kutafuta suluhisho la ndoa hii ili ifungwe licha ya kuchelewa lakini mpaka sasa
hakuna dalili zozote kuwa ndoa hii itafungwa kwani bwanaharusi hajulikani alipo
hivyo nimesitisha ndoa hii na niwaombee ndugu mkafanye jitihada zenu kumtafuta
kijana huyu na mfikie muafaka kwa pande zote mbili ”Alisema Mchungaji.
Amesema
taratibu za ndoa zinataka siku 21 ndoa ifungwe hivyo yeye kama mchungaji
kisheria ndiye mdhamini na mtangazaji wa kisheria kwa suala la ndoa ya mwaka 71
ambayo inampa mamlaka ya kueleza kwanini ndoa haikufungwa kwa siku 21 kwa
mujibu wa sheria.
Bibi
harusi atolewa kanisani akiwa amevuliwa shera …………………
Katika
kile ambacho kilisubiliwa kwa hamu na ndugu na jamaa kuona hitimisho la ndoa
hiyo ambapo bibi harusi aliingizwa katika gari maalumu bila kuvalishwa
shera pamoja na kufunikwa kanga na kuondoka kanisani hapo majira ya saa 10
jioni wakielekea pasipo julikana huku baadhi ya ndugu wakionesha majonzi na
wengine kutokwa na machozi kwa kutoa amni kile kilichotokea .
Waliochanga
kwa ajili ya sherehe ya usiku……………
Mara
baada ya sinema hiyo kukamilika kanisani ndugu na jamaa waliochanga pesa zao
kwa ajili ya kuhudhuria sherehe ya usiku walianza kueleza kuwa watafika
ukumbini kama kawaida na kula chakula na kunywa ili kufidia pesa yao.
Sherehe
hiyo ilipangwa kufanyika katika Ukumbi wa Mkapa Hall jijini Mbeya na
kuhudhuriwa na watu zaidi ya mia tatu ambapokila kwa michango wanakamati
ilikuwa laki moja na wengine shilingi elfu 70.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “BWANAHARUSI AINGIA MITINI MUDA MCHACHE KABLA YA NDOA JIJINI MBEYA ”
Post a Comment