Friday, December 16, 2016
KAMA HUNA CHOO JIANDAE SERIKALI IMETANGAZA KIAMA KWAKO
Do you like this story?
Serikali
imesema ifikapo juni tano mwakani itaendesha operesheni nchi nzima ya
kuwakamata na kuwapeleka katika vyombo vya sheria kaya ambazo zitabainika kuwa
zimeshindwa kuwa na vyoo bora kutokana na utafiti kubaini kaya ambazo zina vyoo
bora nchini ni chini ya asilimia 20.
Kwa
mujibu wa waziri wa afya, maendeleo ya jamii. jinsia, wazee na watoto hali hiyo
inatokana na takwimu kubaini kuwa ni 19 tu ya wakazi wa mijini wana vyoo bora
huku asilimia kumi tu ya wakazi wa vijijini wakitumia vyoo bora na tayari muda
wa miezi sita uliotolewa na serikali kwa kaya zote kuwa na vyoo hivyo unazidi
kwenda.
Waziri
Ummy Mwalimu ameweka msisitizo huo wakati akizindua ripoti ya matokeo ya
utafiti wa afya ya uzazi na mtoto na viashiria vya Malaria na kusema kuwa kamwe
hawezi kuvumilia watanzania wakiendelea kuumwa magonjwa yanayozuilika yakiwemo
yale yanayosababishwa na ukosefu wa vyoo bora.
Naye
mkurugenzi mkuu wa ofisi ya Taifa ya takwimu Dr. Albina Chuwa amesema wamefanya
utafiti huo ili kuweza kuyabaini yanayojiri katika sekta ya afya na kuiwezesha
serikali kubaini madhaifu yaliyopo sambamba na kubuni mikakati ya kutatua
changamoto hizo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ KAMA HUNA CHOO JIANDAE SERIKALI IMETANGAZA KIAMA KWAKO”
Post a Comment