Friday, December 16, 2016
SERIKALI YAPIGA MARUFUKU SIASA MASHULENI
Do you like this story?
Serikali
imepiga marufuku siasa kuingilia utekelezaji wa majukumu ya kitaaluma kwenye
sekta ya elimu na kuwaagiza wakurugenzi na makatibu tawala wa halmashauri miji
na majiji kuwalinda na kuwasaidia walimu wakuu na wakuu wa shule watakaoripoti
kubugudhiwa na wanasiasa kwa namna yeyote ile.
Agizo
hilo linatolewa na wizara ya elimu sayansi teknolijia na mafunzo ya ufundi
Profesa Joyce Ndalichako katika mkutano na wajumbe wa shirikisho la wakuu wa
shule za sekondari nchini TAHOSSA ambao awali walimueleza Mhe waziri kuwa hivi
sasa wanashindwa kutekeleza majukumu yao ipasvyo kutokana na kuhofia wanasiasa
ambao wamefikia hatua hata ya kuwaadhibu.
Mbali
na changamoto hiyo ya wanasiasa wakuu hao washule pia wakabainisha matatizo
lukuki wanayokumbana nayo ikiwemo mazingira mabovu ya kazi ukosefu wa walimu,
vifaa vya kujifunza na kufundishia huku wakiiomba serikali kuruhusu ajira kwa
walimu kwani kuna uhaba mkubwa hasa maeneo ya vijijini.
Nao
wadau wa elimu walioshiriki kwenye mkutano huo wamesema imefika wakati sasa
elimu inayotolewa nchini kuwaandaa wanafunzi wanaohitimi elimu katika ngazi
mbalimbali kuondokana na fikra za kuajiriwa badala yake wajiajiri kwani nchi
nyingi zilizopiga hatua walitumia mfumo huo.
Katika
mkutano huo pia wakuu hao wa shule wakatoa tuzo kwa wadau mbalimbali ambao
mchango wao umetambulika katika kusaidia elimu kusonga mbele.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “SERIKALI YAPIGA MARUFUKU SIASA MASHULENI”
Post a Comment