Monday, December 5, 2016
SERIKALI YAITAMBUA RASMI MITANDAO YA KIJAMII (BLOGGERS)
Do you like this story?
Bloggers wakifuatilia mada. |
Serikali imetangaza rasmi kuitambua mitandao ya
Kijamii (Bloggers) kuwa chombo cha habari nchini.
Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Idara ya Habari
Maelezo na Msemaji wa Serikali Dk.Hassan Abbas Dar es Salaam leo wakati
akifungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Tanzania Bloggers Network (TBN).
“Serikali sasa inaitambua rasmi mitandao ya kijamii
kuwa ni chombo cha habari kama ilivyo vyombo vingine nchini hivyo nawaomba
wakuu wa vitengo vya habari serikalini kushirikiana na wanamitandao hiyo katika
kutoa taarifa mbalimbali” alisema Abbas.
Abbas alivitaka vyombo vya habari hasa magazeti pale
wanapotumia picha kutoka mitandao ya kijamii kueleza chanzo cha picha hiyo
tofauti na ilivyo hivi sasa ambapo picha zao zinatumika bila ya kutaja chanzo.
Katika hatua nyingine Abbas alisema Bloggers haina
tofauti na vyombo vingine hivyo ni vema wanapotoa habari zao kuzingatia sheria
na weredi wa kazi vinginevyo sheria itawakumba kama ilivyo kwa magazeti na
vyombo vingine.
Abass aliwataka wanamitandao hao kujiunga na TBN ili
iwe rahisi kutatuliwa changamoto walizonazo kuliko kila mmoja kuwa kivyake.
Wanamitandao hao wakizungumzia changamoto waliyonayo
walimwambia mkurugenzi huyo kuwa wamekuwa wakibaguliwa na maofisa habari
wa serikalini ikiwa pamoja na kunyimwa ‘Press Card’ jambo linalokwamisha
utendaji wao wa kazi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “SERIKALI YAITAMBUA RASMI MITANDAO YA KIJAMII (BLOGGERS)”
Post a Comment