Tuesday, March 25, 2014

DIAMOND AENDELEA KUPETA TUZO ZA KILI, ATENGEWA TUZO SITA 2014.




MWANAMUZIKI nyota nchini, Nassib Abdul 'Diamond Platinum' ameingia katika vipengele sita vya kinyan’ganyiro cha tuzo za muziki nchini, maarufu kama Kilimanjaro Tanzania Music Awards 2014.

Kwenye muziki mama (dansi na taarab) kuna mchuano mkali katika vipengele vya mwimbaji bora, mtunzi bora, mwimbaji bora wa kiume, mwimbaji bora wa kike, kundi bora na bendi bora.

Katika wimbo bora wa bendi Ushamba Mzigo (Mashujaaa Band), Shamba la Bibi (Victoria Sound), Chuki ya Nini (FM Academia), Yarabi Nafsi (Mapacha Watatu) na Kiapo Mara Tatu (Talent Band) zitachuana vikali huku kwenye wimbo bora wa taarab kutakuwa na Wasi wasi wako – Mzee Yussuf,  Nipe Stara – Rahma Machupa, Sitaki Shari – Leyla Ramadhan, Mambo Bado – Hadija Yussuf  (wote Jahazi Jahazi), Asiyekujua Hakuthamini – Isha Ramadhan na Saida Ramadhan (Mashauzi Classic), Fahari ya Mwanamke – Hadija Kopa (G5 Modern Taarab), Kila Muomba Mungu – Mwanahawa Ali (Five Stars Modern Taraab).

Katika bendi bora za dansi ni Bendi ya mwaka , FM Academia, Mapacha Watatu, African Stars(Twanga Pepeta), Akudo Impact, Malaika Band, Mashujaa Band wakati kundi bora la taarab ni mchuano kati ya Jahaz Modern Taarab Mashauzi Classic na Five Stars.

Pata wasaa wa kujionea mwenyewe vipenge vyote. Vipengele vilivyozidi washiriki watano imetokea kwa sababu ya watu kufungana kura wakati zile zenye pungufu ya tano ni kwasababu ya uchache wa washiriki wanaokidhi vigezo vya mwaka husika. 

Saluti5 imegundua kuwa yapo makosa ya kiaundishi kwenye baadhi ya majina ambapo utakutana na makosa kadhaa katika orodha hii iliyoandaliwa na waandaaji. Kwa mfano kwenye watunzi bora wa taarab utakutana na makosa kama vile Thabit Abdul kuandikwa Sadiki Abdul, Alhad Omar kuandikwa El Ahadi Omar.


Wimbo bora wa mwaka 
1 Number one-Diamond
2 Joto hasira-Lady Jaydee Ft Prof Jay
3 I love u-Cassim Mganga
4 Yahaya-Lady JayDee
5 Kidela -Abdu Kiba Feat Ali Kiba
6 Muziki gani-Ney ft Diamond

Wimbo bora wenye vionjo vya asili ya Kitanzania

1 Kwejaga nyangisha-Batarokota
2 Nalonji-Kumpeneka
3 Bora Mchawi-Dar Bongo massive
4 Tumbo lamsokota-Ashimba
5 Aliponji -Wanakijiji
6 Agwemwana-Cocodo African music band

Wimbo bora wa kiswahili -Bendi

1 Ushamba mzigo-Mashujaa Band
2 Shamba la Bibi -Victoria Sound
3 Chuki ya nini -FM Academia
4 Yarabi nafsi -Mapacha Watatu
5 Kiapo mara 3 -Talent Band

Wimbo bora wa Reggae 

1 Niwe na wewe-Dabo
2 Hakuna Matata-Lonka
3 Tell Me-Dj Aron ft Fidempha
4 Bado nahitaji-Chikaka ft Bless p & Lazzy B
5 Bongo Reggae-Warriors from the east

Wimbo bora wa Afrika Mashashariki

1 Tubonge-Jose Chamelleone
2 Nakupenda Pia-Waire Ft Allain
3 Badilisha-Jose Chamelleone
4 Kipepeo-Jaguar
5 Kiboko Changu-Aman FT Weizal and Radio

Wimbo bora wa Afro pop 

1 Number one-Diamond
2 Joto hasira-Jay Dee
3 Kidela-abdul kiba ft Ali Kiba
4 I love you-Kassimu
5 Tupogo-Ommy Dimpoz Ft J Martins
6 Roho yangu-Rich Mavoko

Wimbo bora wa Taarab 

1 Wasi wasi wako-Mzee Yusuf
2 Asiyekujua Hakuthamini-Isha Ramadhani & Saida Ramadhani
3 Nipe stara -Rahma Machupa
4 Sitaki shari-Leyla Rashid
5 Fahari ya Mwanamke-Khadija Kopa
6 Mambo bado-Khadija Yusuf
7 Kila muomba Mungu -Mwanahawa Ali

Wimbo bora wa Hip hop 

1 Bei ya mkaa-Weusi
2 Nje ya box-Nick wa pili ft Joh Makini and , Gnako
3 Siri ya mchezo-Fid q ft Nature
4 2030-Roma
5 Pesa-Mr Blue Ft Becka Title

Wimbo bora wa R&B 

1 Listen-Belle 9
2 Closer -Vanessa Mdee
3 So crazy-Maua ft Fa
4 kama huwezi-rama dee ft jay dee
5 Wa ubani-Ben Pol ft. Alice

Wimbo bora wa kushirikisha/kushirikiana

1 Music Gani-Ney Mitego ft Diamond
2 Joto Hasira-Lady JayDee ft. Prof Jay
3 Kidela -Abdul Kiba ft. Ali Kiba
4 Bila Kukunja Goti-Mwana FA na AY ft. Jay Martins
5 Tupogo-Ommy Dimpoz ft. Jay Martins

Wimbo bora wa Ragga/Dancehall 

1 Nishai-Chibwa Ft Juru
2 Sex girl-Dr Jahson
3 My sweet-Jettyman Dizano
4 Feel Alright-Lucky Stone
5 Wine-Princess Delyla

Wimbo bora wa Zouk /Rhumba

1 Yahaya-Lady Jaydee
2 Yamoto-Mkubwa na wanawe
3 Msaliti-Christian Bella
4 Nakuhitaji-Malaika Band
5 Narudi kazini-Beka

Mwimbaji bora wa kike -kizazi kipya

1 Vanessa Mdee
2 Lady Jaydee
3 Linah
4 Maua

Mwimbaji bora wa kiume -kizazi kipya

1 Ben Pol
2 Rich Mavoko
3 Diamond
4 Ommy Dimpoz
5 Cassim Mganga

Mwimbaji bora wa kike -Taarab

1 Khadija Kopa
2 Isha Ramadhani
3 Khadija Yusuf
4 Mwanahawa Ali
5 Leyla Rashid

Mwimbaji bora wa kiume -Taarab

1 Mzee Yusuf
2 Hashimu Saidi
3 Mohamedi Ali aka Mtoto Pori

Mwimbaji bora wa kiume -Bendi

1 Jose Mara
2 Kalala Junior
3 Charz Baba
4 Khalid Chokoraa
5 Christian Bella

Mwimbaji bora wa kike -Bendi 

1 Luiza Mbutu
2 Catherine (Cindy)
3 Ciana

Msanii bora wa -Hip hop 

1 FID Q
2 Stamina
3 Young killer (Msodoki)
4 Nick wa pili
5 Gnako

Msanii bora chipukizi anayeibukia

1 Young Killer(Msodoki)
2 Walter Chilambo
3 Y Tony
4 Snura
5 Meninah

Rapa bora wa mwaka -Bendi

1 Kitokololo
2 Chokoraa
3 Furguson
4 Canal Top
5 Totoo ze Bingwa

Mtumbuizaji bora wa kike wa Muziki 

1 Khadija Kopa
2 Vanessa Mdee
3 Isha Ramadanni
4 Luiza Mbutu
5 Catherine (Cindy)

Mtumbuizaji bora wa kiume wa Muziki

1 Diamond
2 Christian Bella
3 Rich Mavoko
4 Ommy Dimpoz
5 Abdu Kiba

Mtayarishaji bora wa nyimbo wa mwaka -Taarab

1 Enrico
2 Ababuu Mwana ZNZ
3 Bakunde

Mtayarishaji bora wa nyimbo wa mwaka -Kizazi kipya

1 Marco chali-Mj Records
2 Man Water-Combination Sound
3 Mazoo-Mazoo Records
4 Sheddy Clever-Burnz Records
5 Nahreel -Home Town Record

Mtayarishaji bora wa nyimbo wa mwaka -Bendi

1 Allan Mapigo
2 C9
3 Enrico
4 Amoroso
5 Ababuu Mwana ZNZ

Mtunzi bora wa mwaka -Taarabu

1 Mzee Yusuf
2 El-Ahad Omary
3 El-khatib Rajab
4 Kapten Temba
5 Sadiki Abdul
6 Nassoro Seif

Mtunzi bora wa mwaka -kizazi kipya

1 Belle 9
2 Ben Pol
3 Diamond
4 Rama dee
5 Rich mavoko

Mtunzi bora wa mwaka -Bendi

1 Christia Bella  
2 Jose Mara
3 Chaz Baba
4 Nyoshi Saadat
5 Kalala Junior

Mtunzi bora wa mwaka -Hip hop

1 Nikki wa Pili
2 Young Killer(Msodoki)
3 Roma
4 FID Q
5 G- Nako
Video bora ya muziki ya mwaka
1 Number one-Diamond
2 Yahaya-lady Jaydee
3 Joto hasira-Lady Jaydee Ft Prof Jay
4 Uswazi takeaway-Chege Ft Malaika
5 Mama Yeyo-Gnako Ft Ben Pol

Bendi ya mwaka 

1 FM Academia
2 Mapacha Watatu
3 African Stars(Twanga Pepeta)
4 Akudo Impact
5 Malaika Band
6 Mashujaa Band

Kikundi cha mwaka cha Taarab

1 Jahaz Modern Taarab
2 Mashauzi Classic
3 Five Stars

Kikundi cha mwaka cha kizazi kipya

1 Makomandoo
2 Navy kenzo
3 Weusi
4 Mkubwa na wanawe

0 Responses to “DIAMOND AENDELEA KUPETA TUZO ZA KILI, ATENGEWA TUZO SITA 2014.”

Post a Comment

More to Read