Saturday, April 26, 2014

CHUO KIKUU MZUMBE CAMPUS YA MBEYA WAUNGANA NA WATOTO YATIMA NCHINI KUSHEREKEA SHEREHE ZA MUUNGANO.



Mkuu wa Chuo Kikuu Cha Mzumbe Campus ya  Mbeya Prof.Kihanga Ernest mwenye Suti Nyeusi akiwa na Mwadhiri  Ladslausi Rwekaza wakiwa wanateta jambo.


Mkuu wa Chuo Kikuu Cha Mzumbe Campus ya  Mbeya Prof.Kihanga Ernest mwenye Suti Nyeusi akiwa na wanafunzi wa chuo hicho pamoja na walimu wao wakiwa chuoni hapo wakijianda kwenda kukabidhi msaada wa mahitaji mbalimbali katika kituo cha watoto yatima kilichopo  Simike jijini Mbeya ikiwa ni sehemu ya kusherekea Sherehe za Muungano



Profesa Kihanga akizungumza na baadhi ya watoto hao kabla ya kukabidhiwa  msaada kwa mama malezi wa kituo hicho.

 Mama mlezi  Bi Anna Kasile wa kituo cha watoto yatima kilichopo Simike Mkoani Mbeya akitoa maelezo


Baadhi ya wanajumuiya hao wakikabidhi msaada kwa mama mlezi wa kituo hicho Bi.Anna Kasile.

Mkuu wa Chuo Kikuu Cha Mzumbe Campus ya  Mbeya Prof.Kihanga Ernest Akiwa na Steven john mwadhiri wakikabidhi kiasi cha pesa shillingi Laki Tano(500,000) pamoja na vitu Mbalimbali.



Jumuiya ya Chuo Kikuu Mzumbe  Cumpus ya Mbeya imeungana watoto yatima Mkoani Mbeya na Baadhi ya maeneo Mengine Nchini Katika Kusherekea  Kilele cha Sherehe za Muungano.

Jumuiya hiyo ambayo ni mchanganyiko wa wanafunzi walimu  na watumishi wote wa chuo hicho wameungana kwa pamoja na kutoa msaada wa chakula pamoja na mahitaji mengine katika kituo cha kulelea watoto yatima cha Malezi ya Huruma kilichopo Simike jijini Mbeya msaada wenye thamani ya zaidi ya shilingi mil2.

Akikabidhi Msaada huo kwa niaba ya wanajumuiya hao Mkuu wa chuo cha Mzumbe Campus ya Mbeya Prof.Kihanga Ernest amesema hatua ya kutimiza miaka 50 ya muungano wa Tanzania ni furaha kubwa  hivyo wao wameamua kufurahi na watoto wanaoishi katika mazingira magumu.

Amesema isingekuwa vyema kusherekea sherehe hizo wakati kuna watu wanaishi katika mazingira magumu na wanahitaji msaada kwa mahitaji  mbalimbali hivyo msaada huo ni sehemu ya kuifanya jamii kama hiyo kuwa kwa pamoja katika sherehe hizo.

Hata hivyo profesa huyo amesema katika muungano huo umekuwa na amani kubwa sana hivyo hata vijana hao wanapaswa kufurahi na kuiona faida hiyo ili nao waweze kujua historia na hatimaye kuendelea kuulinda muungano huo.

Pamoja na muungano huo kudumu kwa miaka 50 lakini pia umetoa fursa kwa vijana kupata elimu  Uzanzibari na Utanganyika pamoja na kuitangaza vyema Tanzania Kimataifa kama sehemu ya Amani .

Aidha Profesa huyo amelitaka bunge la katiba kuangalia  kwa umakini suala kuulinda muungano huo kwa kuhakikisha linaingia katika Katiba mpya.

Aidha Kwa upande wake Mratibu wa shughuli hizo ambaye pia ni Mhadhiri wa chuo hicho Ndugu Steven John amesema kuwa tofauti na kusherekea miaka 50  ya  Muungano lakini pia wameona washilikiane na jamii ili isionekane kuwa chuo kikuu ni sehemu ya kusoma tu badala yake iwe sehemu ya jamii.

Amesema  wameamua kuonyesha mjumuiko wao na watu wanaowahitaji   ili kuweza kuleta nuru ya siku ya muungano kwani wanaamini yapo mengi wanayohitaji lakini kwa kufanya hivyo kutaleta faraja kubwa kwa kundi hilo.

Amesema msaada uliotolewa na wanajumuiya hao ni michango toka katika mifuko yao binafsi bila kuhusisha taasisi hiyo  ya Mzumbe .

Akipokea msaada huo Mama mlezi wa kituo hicho Ndugu Anna kasile amesema msaada uliotolewa na wanajumuiya hao umefika katika siku muafaka hasa kutokana na kuwepo kwa uhaba wa chakula katika kituo kilichopo Morogoro ambacho nacho kipo chini yake.

Amesema msaada huo utagawanywa ambapo chakula kingine kitasafirishwa  na kupelekwa mkoani morogoro hivyo amewashukuru wanajumuiya hao kwa kuonyesha moyo huo.

Amesema katika kituo hicho cha Simike kinajumla ya watoto 120 ambao wanahitaji gharama kubwa katika kuwahudumia hivyo msaada huo unawasaidia kwa kiasi kikubwa.

0 Responses to “CHUO KIKUU MZUMBE CAMPUS YA MBEYA WAUNGANA NA WATOTO YATIMA NCHINI KUSHEREKEA SHEREHE ZA MUUNGANO.”

Post a Comment

More to Read