Thursday, March 27, 2014
KUHUSU SAKATA LA WATANZANIA KUFANYISHWA UKAHABA CHINA, WAZIRI MEMBE ATOA KAULI.
Do you like this story?
WIZARA
ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, imebaini kuwepo mtandao wa
wanaosafirisha wasichana wenye umri mdogo kutoka nchini na kuwapeleka China
kisha kuwafanyisha vitendo vya ukahaba pasipo ridhaa yao.
Hayo
yalisemwa jijini Dar es Salaam jana na Waziri wa Wizara hiyo, Bernard Membe,
wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na masuala mbalimbali
yanayohusu wizara yake.
Alisema
mtandao huo ukishasafirisha wasichana hao na kuwafikisha China, huwanyang'anya
hati zao za kusafiria na kujikuta wakishindwa kurejea nyumbani, hali
inayowalazimisha kujikuta wakitumbukia kwenye biashara hiyo.
Membe
alisema, taarifa ambazo wizara yake inazo ni kwamba, tayari mmoja wa wasichana
hao amefariki kwa kuuawa. Alisema mwezi uliopita walialikwa kwenda nchini
China, ambapo walibaini kuwepo kwa vitendo hivyo vya kusafirisha wasichana
kutoka Tanzania na kuwapeleka nchini humo ili kuwafanyisha ukahaba.
"Inaelekea
kuna Watanzania wanaokwenda nchini China kwa kutumia nyaraka bandia, huku
wengine wakitumia paspoti ya nchi zingine wakati wao ni Watanzania ili kusafiri
nje ya nchi kwa lengo la kufanya biashara ambazo ni haramu," alisema
Membe.
Alisema
kutokana na kukithiri kwa hali hiyo, Rais Jakaya Kikwete, atakuwa na ziara ya
kutembelea nchi hiyo ambapo pamoja na mambo mengine ataenda kujionea hali
halisi ya kuwepo kwa vitendo hivyo.
Kwa
mujibu wa Waziri Membe, zaidi ya Watanzania milioni 3 wanaishi nje ya nchi,
lakini baadhi yao wapo wanaofanya ukabaha, biashara za dawa za kulevya na
ugaidi. "Kufanya vitendo hivyo ni kuivunjia heshima nchi yetu,"
alisema na kuwataka Watanzania wasirubuniwe kwenda nje ya nchi kwa kudhani kuwa
maisha ya huko ni rahisi.
Aliwataka
wenye mitandao ya kuendesha madanguro ya ukahaba nje kwa kutumia wasichana wa
Kitanzania wajue kwamba kufanya hivyo ni kosa la jinai. Aliwataka Watanzania
wanaoishi huko waishi kwa kufuata misingi ya nchi na taratibu husika ili
kulinda heshima ya nchi.
Wakat
i huo huo, Waziri Membe alisema wizara yake kwa kushirikiana na Mkuu wa Jeshi
la Polisi Nchini, IGP Ernest Mangu, watatuma timu kwenda nchini humo ili
kutambua watu wanaoendesha biashara hiyo ili kuikomesha.
Katika
hatua nyingine, Waziri Membe, alisema Tanzania imekubali kupeleka wanajeshi
wake Sudan Kusini kwa ajili ya kushiriki wengine kulinda amani. Alisema
Tanzania imefikia hatua hiyo baada ya kuombwa kutokana na kazi nzuri ambayo
wanajeshi wa JWTZ wamefanya nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).
"Kwa
sasa hivi maandalizi hayo yapo katika hatua za mwisho na Tanzania itaendelea
kuimarisha diplomasia ya ushirikiano baina ya nchi jirani katika kulinda na
kudumisha amani,"alisema Membe.
Kwa
upande wa mgogoro, alisema Juni, mwaka huu ujumbe wa Tanzania utakutana na jopo
la usuluhishi wa mgogoro huo kwa lengo la kujadili faida na hasara za mpaka huo
kuwa katikati ya Ziwa Nyasa.
Alisema
mkutano huo ulikuwa ufanyike Mei, mwaka huu,lakini kutokana na Malawi kuwa na
uchaguzi, mkutano huo umesogezwa mbele.
Akizungumzia
uhusiano wa Tanzania na Rwanda, Waziri Membe, alisema kumekuwa na msuguano sana
baina ya nchi hizo, lakini Tanzania haina ugomvi na majirani zake.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “KUHUSU SAKATA LA WATANZANIA KUFANYISHWA UKAHABA CHINA, WAZIRI MEMBE ATOA KAULI.”
Post a Comment