Thursday, March 27, 2014
MKENYA ATUHUMIWA KUIKOSESHA MAPATO TCRA.
Do you like this story?
Raia wa Kenya nelson
rading onyango amefikishwa mahakama ya hakimu mkazi kisutu
dare s salaam akikabiliwa na
mashitaka saba ikiwamo la kutoa huduma
ya mawasiliano ya kimataifa bila ya kuwa na leseni na kulisababisha taifa hasara ya zaid y ash
6.8 bilioni.
Akisomea hati ya mashtaka
wakili mwandamizi wa serikali tumaini kweka alidai jana kuwa kati ya julai 2010 na November 2013 katika eneo la kariakoo mshitakiwa alifanya udanganyifu matumizi ya mtandao
kinyume cha sheria.
Kweka alidai kuwa mshtakiwa
kwa nia ya udanganyifu alikuwa akiendesha huduma za mawasiliano ya kimtaifa huku akikwepa kutumia njia halali
za malipo zinapotolewa na mamlaka ya
mawasiliano Tanzania(TCRA)
Katika shitaka la
pili anadaiwa kutoa huduma
ya mawasiliano bila ya kuwa na
leseni wakili huyo wa serikali alidai kuwa katika kipindi hicho mshtakiwa bila
ya kuwa na uhalali kisheria alito a huduma ya simu za kiamtaifa bila ya kuwa na leseni inayotolewa na TCRA .
Katika shitaka la tatu
anadaiwa kuwa kati ya January 2013 na
November 2013 akiwa katika eneo la kariakoo alitumia kadi za simu zisizo sajiliwa.
Katika shitaka la nne
anadaiwa kuingiza nchini vifaa vya kielektroniki bila ya kuwa na kibali
kinachomruhusu kufanya hivyo.
Katika shitaka la tano
alidai kuwa licha ya kuingiza nchini mitambo hiyo bila ya kuwa na kibali mshitakiwa huyo alisimika mitambo mine ya mawasiliano na
kuiendesha. Mitamgo hiyo ni SM boxi zenye namba za siri TX 2SN5600C5/05,TX2SN48002/K21,TX2SN1002335A
na cisco router.
Katika shitaka la sita
wakili alidai kuwa onyango alitumia mitambo hiyo ya kielektroniki ambayo ilikuwa haijathibitishwa na TCRA .
Mshtakiwa pia
anadaiwa kusababisha hasara y ash 6.8
bilioni kwa TCRA kati ya julai 2010 na
November 2013 kwa kutoa huduma za mawasiliano
ya kimataifa bila ya kuwa na leseni.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “MKENYA ATUHUMIWA KUIKOSESHA MAPATO TCRA.”
Post a Comment