Thursday, March 27, 2014
MJUMBE AMPA SOMO MWENYEKITI WA BUNGE LA KATIBA.
Do you like this story?
Mjumbe wa bunge la katiba constatine akitanda ameshauri mwenyekiti wa bunge la katiba Samuel sitta azibe masikio kwa chama chake
ili aweze kulipeleka taifa mahali
salama.
Akitanda amesema hayo katika
mahojiano maalumu yaliyofanyika Dodoma juzi.
Kwa jinsi sitta anavyoliendesha bunge hilo asifikiri kuwa ni njia sahihi bali
anachochea wajumbe hasira wakati katiba
ni suala la maridhiano alisema.
Mwenyekiti anayo nafasi ya
kulpeleka taifa mahali salama kwa kuziba
masikio kwa chama chake najua ni vigumu lakini inawezekana kufanya hivyo kwa kuendesha bunge kidemokrasia.
Alimtaka sitta akumbuke
kuwa mapendekezo ya katiba yatapelekwa
kwa wananchi kwa ajili ya kupigiwa kura
na kwamba wananchi wanajua pumba na mchele ni ufupi kwa sababu wanaona na
kusikia.
Ni heri majina yetu
yaandikwe kwa masizi yafutike baada ya muda mfupi kuliko kukubali kuburutwa
na majina kuandikwa kwa wino wa dhahabu alisema akitanda.
Kuhusu muundo wa serikali
akitanda alisema ni ukweli kwamba
Tanzania kumekuwa na kero za
muungano kwa miaka 50 ambazo
hazijatulika lakinijambo la kujiuliza ni kama seikali tatu ama mbili zinatoa
majibu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “MJUMBE AMPA SOMO MWENYEKITI WA BUNGE LA KATIBA.”
Post a Comment