Thursday, March 27, 2014
NILIMHUDUMIA TUPPA KWA DAKIKA 25.
Do you like this story?
Mganga mkuu wa hospitali
ya halmashauri ya wilaya ya tarime
marco nega amesema walimpokea mkuu wa mkoa wa mara john tuppa akiwa mahututi na alifariki dakika 25 za matibabu.
DK nega alisema tayari
walikuwa wamejiandaa kumpatia matibabu
kwa sababu walipewa taarifa
mapema kwamba hali yake ni mbaya baada ya
kubadilika ghafla, akipewa taarifa na mkuu wa wilaya ya tarime john henjewele.
Amesema walimpokea tuppa saa 3:45 asubuhi
na kwamba baada ya mapokezi walichukua vipimo na kukuta ni shinikizo la
damu likiwa juu kwa kiwango cha 160/
140.
Kwa mujibu wa
mwanasanyansi wa tiba ya binadamu Samuel shita kiwango cha peresha cha 160/140
mmhg ni shinikizo kali la damu.
Uhatari huo anauelezea ni
mbaya zaidi kutokana na namba ya chini 140 ambayo kwa kawaida inapaswa
kuwa kati ya 60 na 90.
Dk nega alisema wakati
wakiendelea kujaribu kushusha shinikizo hilo kali ilipotimu saa 4:15 asubuhi
alifariki dunia.
Tulipigiwa simu kutoka ofisi ya DC(Mkuu wa wilaya) kuwa
mkuu wa mkoa analetwa kwa matibabu tukijiweka tayari kwakweli alifikishwa akiwa mahututi hajitambui alisema DK nega na kuongeza
alikutwa (Tuppa) na shinikizo la damu iliyokuwa juu kwa hiyo tulimpokea akiwa
mzima angekuwa amekufa tusingebaini ugonjwa huo maana mtu aliyekufa vipimo
havionyeshi.
Baadhi ya wajumbe walikuwa
kwenye kikao walieleza kuwa mkuu wa mkoa wakati anasomewa taarifa ghafla hali yake ilibadilika na kuanguka chini ka
kutokwa na mapovu mdomoni.
Mmoja wa wajumbe wa kamati
ya ulizni na usalama alisema tuppa alikuwa mzima lakini walishangaa ghafla
akiwa mekaa kwenye kiti alianza kuhema kwa nguvu kabla ya kuishiwa nguvu.
Katibu tawala mkoa wa mara
bendicto ole kuyan ametoa ratiba awali ya kusafirisha na mazishi ya aliyekuwa
mkuu wa mkoa wa mara john tuppa.
Ratiba hiyo inaonyesha
mwili huo utaagwa leo nyumbani kwake
ikulu ndogo musoma kuanzia saa 1:30
asubuhi hadi 3:20 asubuhi.
Kuyan amesema baada ya
kuagwa saa 3:25 asubuhi mwili utapelekwa kanisani katoliki jimbo la musoma kwa ajili ya ibada ya wafu
itakayongozwa na askofu Michael msonganzila.
Amesema baada ya ibada saa
5:00 asubuhi mwili utasafirishwa kuelekea uwanja wa ndege mwanza kwa ajili ya kuelekea Dodoma.
Kuyan amesema kesho
kuanzia saa 3:00 asubuhi hadi 6:00 mchana viongozi na wnanchi wa Dodoma wataaga
mwili huo kutokana viongozi kuokba kuaga
hapo kwa asababu aliwahi kufanya kazi Dodoma.
Ameseme machi 29 kuanzia
saa 3:00 asubuhi itafanyika ibada nyumbani kwake kilosa na wananchi kuaga mwili kasha kupelekwa eneo
la maziko.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “NILIMHUDUMIA TUPPA KWA DAKIKA 25.”
Post a Comment