Wednesday, March 26, 2014
SAMWEL SITTA ASISITIZA KUWA BUNGE LA KATIBA LITATUMIA MUDA ULIOPANGWA.
Do you like this story?
Mwenyekiti
wa Bunge Maalum la Katiba, Samuel Sitta, amewataka wajumbe wa Bunge hilo
kutambua kuwa muda wa kuwapo kwa Bunge hilo umewekwa kisheria, hivyo inabidi
kazi ya kutunga Katiba imalizike ndani ya muda uliopangwa.
Sitta
aliyasema hayo jana baada ya baadhi ya wajumbe kuonyesha kutoridhishwa na kauli
yake ya kutaka baadhi ya sura zaidi ya moja za Rasimu ya Katiba ambazo siyo
muhimu kujadiliwa kwa siku moja. "Waheshimiwa wajumbe tuelewe kwamba muda
wetu wa kuwa hapa bungeni umepangwa kisheria kwamba ni siku 70 tu,
zitakapokwisha inabidi tumalize ili taifa liendelee na shughuli nyingine,"
alisema Sitta.
Awali
Sitta aliwaeleza wabunge kuwa baadhi ya Sura za Rasimu ya Katiba ambazo
hazihitaji marekebisho makubwa itabidi zijadiliwe mbili au tatu kwa pamoja
katika siku moja, ili kuokoa muda, kauli ambayo iliibua minong'ono kutoka kwa
baadhi ya wajumbe wa Bunge hilo, wakidhani kuwa Mwenyekiti anataka kuwaburuza.
Kwa
mujibu wa Sheria namba nane ya Mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2011 Bunge Maalum
la Katiba limepangiwa siku 70 ambazo zinaweza kuongezwa hadi kufikia siku 90
muda ambao Bunge hilo linatakiwa kuwa limekamilisha kazi yake.
Hata
hivyo, bado kuna mkanganyiko wa lini Bunge Maalum lilianza kwa mujibu wa
sheria, hali ambayo limfanya Mjumbe wa Bunge hilo, Ezekiel Oluoch kuomba
mwongozo wa Mwenyekiti akitaka aelezwe kama siku za uhai wa Bunge hilo zilianza
kuhesabiwa baada ya kuchaguliwa kwa Mwenyekiti wa kudumu au tangu wakati ule wa
Mwenyekiti wa Muda, Amer Pandu Kificho, aliyekuwa akisimamia uandaaji wa Kanuni
za Bunge hilo.
Akimjibu
Oluoch, Sitta alisema atatoa mwongozo huo baada ya kuwasiliana na wanasheria
wakuu wa Serikali ya Muungano na ile ya Zanzibar ili kupata uhakika wa muda
rasmi wa Bunge hilo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “SAMWEL SITTA ASISITIZA KUWA BUNGE LA KATIBA LITATUMIA MUDA ULIOPANGWA.”
Post a Comment