Wednesday, March 19, 2014
SHIBUDA AMWANGUKIA JK KUHUSU MUUNGANO.
Do you like this story?
Rais Jakaya Kikwete, ameombwa katika hutuba yake ya
kuzindua Bunge la Katiba, atoe msimamo wake juu ya Muundo wa Muungano, badala
ya kuwa na msimamo wa makundi ya kisiasa.
Akizungumza na Mwananchi, Mjumbe wa Bunge la Katiba,
John Shibuda, alisema hivi sasa ni muhimu kila kiongozi kutoa msimamo
wake na maoni katika masuala ya msingi.
“Tunatarajia rais atambulishe maoni yake,
katika kulitakia mema Taifa na kutoa mwelekeo wa taifa, “ alisema Shibuda.
Rais Jakaya Kikwete anatarajia kulizindua
Bunge la Katiba Ijumaa wiki hii katika mazingira ambayo Bunge lenyewe
limegawanyika kimtazamo kuhusu mambo makuu mawili; upigaji kura na Muungano
wa Tanzania. Wakati Chama Tawala CCM kikitaka kura zipigwe kwa uwazi na
muundo wa Muungano uwe wa serikali mblli, wapinzani wanataka kura zipigwe kwa
siri.
Hata hivyo wapinzani wamegawanyika kuhusu
Muungano wa Tanzania ambapo, Chadema wanataka Muungano wa Serikali tatu na CUF
Serikali ya mkataba.
Katika hatua nyingine Shibuda amesema binafsi
katika muundo wa Muungano, anaunga mkono serikali mbili. Nitatetea msimamo huo
popote na wakati wowote, anasema.
“Katika Bunge hili mimi nitakuwa natoa
msimamo kwa kila ambacho nakiamini na siyo kufuata makundi ya watu,” amesema
Shibuda.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “SHIBUDA AMWANGUKIA JK KUHUSU MUUNGANO.”
Post a Comment