Sunday, March 30, 2014

SPIKA ANNA MAKINDA ATOA DARASA KWA WANAWAKE KUCHANGIA HOJA ZA NGUVU KWENYE BUNGE LA KATIBA.




Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Anne Makinda ametoa changamoto kwa wajumbe wenzake wanawake walio kwenye Bunge hilo, kujenga hoja zenye nguvu zinazohusu masuala yanayohusu wanawake na kuzitetea  kwa sauti moja ili ziweze kupita katika Rasimu ya Katiba. 

Kauli hiyo imetolewa leo na Mhe. Anne ambaye pia ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  wakati akitoa mchango wake  kwa  wajumbe  wa semina ya kujenga agenda muhimu kwa masuala ya kijinsia iliyoandaliwa na Umoja  wa Wabunge  Wanawake wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (TWPG) kwa wajumbe wanawake wa Bunge hilo, iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Pius Msekwa.

“ Ninawaomba  tuwe na hoja zenye nguvu wakati wakuchangia mjdala wa Rasimu ya Katiba . Tukisimama kwa  hoja za nguvu na kutetea vifungu vinavyohusu masuala ya wanawake tunaweza kubadilisha vifungu. 

 Tuzungumzeni hoja tuache kufanya fujo, tusiingie katika malumbano ambayo hayana tija, tuache kuzomea tukifanya hiyo tutakuwa tumejijengea heshima,” alisema Mama Anne.

0 Responses to “SPIKA ANNA MAKINDA ATOA DARASA KWA WANAWAKE KUCHANGIA HOJA ZA NGUVU KWENYE BUNGE LA KATIBA.”

Post a Comment

More to Read